Simba yaibadilishia kikosi Singida

Na Winfrida Mtoi

Kuelekea mechi yao na Singida Fountain Gate, Kocha Msaidizi wa Simba, Seleman Matola amesema kutokana na kucheza mechi kila baada ya siku mbili watakuwa na mabadiliko katika kikosi chao kwani baadhi ya wachezaji wamepewa mapumziko.

Matola amesema hayo leo Machi 11,2024 wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maandalizi ya mchezo huo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, utakaochezwa kesho kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi.

“Kwa sababu ukingali ‘game’ zipo kila baada ya siku mbili kwa hiyo nafikiri  kunaweza kuwa na mabadiliko kutokana na kuwapa baadhi ya wachezaji mapumziko, sisi kama benchi la ufundi tutaangalia ni nani anaweza kutufaa katika mchezo wa kesho,” amesema Matola.

Aidha amesema morali yao ipo juu na bado wana nafasi kubwa ya kufanya vizuri katika ligi kuu na kuahidi kuwafurahisha mashabiki wa timu hiyo.

Amekiri kuwa walifanya makosa katika michezo miwili iliyopita dhidi ya Tanzania Prisons Coastal Union  kwa kuruhusu mabao lakini wameshajirekebisha mazoezini.

Katika mchezo uliopita Wekundu wa Msimbazi hao waliifunga Coastal Union 2-1 kwenye Uwanja wa Mkwakwani Tanga.

spot_img

Latest articles

Kamati ya uratibu ya Mradi wa SOFF yakutana jijini Dodoma

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), kwa kushirikiana na Shirika...

ACT Wazalendo Nungwu yafanya mkutano Mkuu wa Kikatiba, Wajumbe zaidi ya 140 washiriki

Na Mwandishi Wetu KATIBU wa Habari, Uenezi na Mawasiliano kwa Umma wa Chama cha...

Tanesco yawataka wananchi kutofanya shughuli za kiuchumi

📌Ni katika zoezi la ukaguzi wa miundombinu ya umeme Tegeta na Mabibo 📌Yatoa rai kwa...

Rejoinder: Tanga Is Still the Strategic Bet, and Tanzania Can Win It

By Peter C. Mhando, PhD Amani Mrope is right: capital has memory. But memory cuts...

More like this

Kamati ya uratibu ya Mradi wa SOFF yakutana jijini Dodoma

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), kwa kushirikiana na Shirika...

ACT Wazalendo Nungwu yafanya mkutano Mkuu wa Kikatiba, Wajumbe zaidi ya 140 washiriki

Na Mwandishi Wetu KATIBU wa Habari, Uenezi na Mawasiliano kwa Umma wa Chama cha...

Tanesco yawataka wananchi kutofanya shughuli za kiuchumi

📌Ni katika zoezi la ukaguzi wa miundombinu ya umeme Tegeta na Mabibo 📌Yatoa rai kwa...