Simba yaibadilishia kikosi Singida

Na Winfrida Mtoi

Kuelekea mechi yao na Singida Fountain Gate, Kocha Msaidizi wa Simba, Seleman Matola amesema kutokana na kucheza mechi kila baada ya siku mbili watakuwa na mabadiliko katika kikosi chao kwani baadhi ya wachezaji wamepewa mapumziko.

Matola amesema hayo leo Machi 11,2024 wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maandalizi ya mchezo huo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, utakaochezwa kesho kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi.

“Kwa sababu ukingali ‘game’ zipo kila baada ya siku mbili kwa hiyo nafikiri  kunaweza kuwa na mabadiliko kutokana na kuwapa baadhi ya wachezaji mapumziko, sisi kama benchi la ufundi tutaangalia ni nani anaweza kutufaa katika mchezo wa kesho,” amesema Matola.

Aidha amesema morali yao ipo juu na bado wana nafasi kubwa ya kufanya vizuri katika ligi kuu na kuahidi kuwafurahisha mashabiki wa timu hiyo.

Amekiri kuwa walifanya makosa katika michezo miwili iliyopita dhidi ya Tanzania Prisons Coastal Union  kwa kuruhusu mabao lakini wameshajirekebisha mazoezini.

Katika mchezo uliopita Wekundu wa Msimbazi hao waliifunga Coastal Union 2-1 kwenye Uwanja wa Mkwakwani Tanga.

spot_img

Latest articles

Ndejembi: Tanzania sasa ina umeme wa kutosha

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amesema Tanzania kwa sasa ina umeme...

Jeshi la Polisi lachunguza  taarifa ya OCD  Chunya

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi limesema limeona na linafanyia uchunguzi taarifa inayosambaa kwenye mitandao...

Uwanja wa Mkwakwani wafungiwa

Na Mwandishi Wetu SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF), limeufungia Uwanja wa Mkwakwani, Tanga kutumika kwa...

Tuzo za TFF za msimu wa 2024/25 zayeyuka

Na Mwandishi Wetu Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limetoa taarifa ya kuahirisha hafla ya utoaji...

More like this

Ndejembi: Tanzania sasa ina umeme wa kutosha

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amesema Tanzania kwa sasa ina umeme...

Jeshi la Polisi lachunguza  taarifa ya OCD  Chunya

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi limesema limeona na linafanyia uchunguzi taarifa inayosambaa kwenye mitandao...

Uwanja wa Mkwakwani wafungiwa

Na Mwandishi Wetu SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF), limeufungia Uwanja wa Mkwakwani, Tanga kutumika kwa...