Simba yaibadilishia kikosi Singida

Na Winfrida Mtoi

Kuelekea mechi yao na Singida Fountain Gate, Kocha Msaidizi wa Simba, Seleman Matola amesema kutokana na kucheza mechi kila baada ya siku mbili watakuwa na mabadiliko katika kikosi chao kwani baadhi ya wachezaji wamepewa mapumziko.

Matola amesema hayo leo Machi 11,2024 wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maandalizi ya mchezo huo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, utakaochezwa kesho kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi.

“Kwa sababu ukingali ‘game’ zipo kila baada ya siku mbili kwa hiyo nafikiri  kunaweza kuwa na mabadiliko kutokana na kuwapa baadhi ya wachezaji mapumziko, sisi kama benchi la ufundi tutaangalia ni nani anaweza kutufaa katika mchezo wa kesho,” amesema Matola.

Aidha amesema morali yao ipo juu na bado wana nafasi kubwa ya kufanya vizuri katika ligi kuu na kuahidi kuwafurahisha mashabiki wa timu hiyo.

Amekiri kuwa walifanya makosa katika michezo miwili iliyopita dhidi ya Tanzania Prisons Coastal Union  kwa kuruhusu mabao lakini wameshajirekebisha mazoezini.

Katika mchezo uliopita Wekundu wa Msimbazi hao waliifunga Coastal Union 2-1 kwenye Uwanja wa Mkwakwani Tanga.

spot_img

Latest articles

Wizara ya Madini na CRDB wasaini makubaliano kurahisisha mikopo kwa wachimbaji wadogo

Na Mwandishi Wetu WIZARA ya Madini kupitia Tume ya Madini leo Februari 23, 2026...

Serikali yatoa Bilioni 8 kujenga Kituo cha Umeme Imalilo-Simiyu

📌 Kituo cha Imalilo kukamilika Mei 2026, kuimarisha ubora wa umeme Bariadi 📌 Serikali yatoa...

Tanzania yaandika historia Mpya: Mradi wa Umeme Jua Kishapu wakamilika

📌 Jumla ya Megawati 50 kuingizwa kwenye Gridi ya Taifa ifikapo Machi 1, 2026 📌...

Kamati ya Bunge Nishati na Madini yaridhishwa na hali ya uzalishaji umeme

📌Yasema jumla ya megawati 4,400 za umeme zinazalishwa kupitia vyanzo mbalimbali 📌Yaipongeza TANESCO...

More like this

Wizara ya Madini na CRDB wasaini makubaliano kurahisisha mikopo kwa wachimbaji wadogo

Na Mwandishi Wetu WIZARA ya Madini kupitia Tume ya Madini leo Februari 23, 2026...

Serikali yatoa Bilioni 8 kujenga Kituo cha Umeme Imalilo-Simiyu

📌 Kituo cha Imalilo kukamilika Mei 2026, kuimarisha ubora wa umeme Bariadi 📌 Serikali yatoa...

Tanzania yaandika historia Mpya: Mradi wa Umeme Jua Kishapu wakamilika

📌 Jumla ya Megawati 50 kuingizwa kwenye Gridi ya Taifa ifikapo Machi 1, 2026 📌...