Simba yaibadilishia kikosi Singida

Na Winfrida Mtoi

Kuelekea mechi yao na Singida Fountain Gate, Kocha Msaidizi wa Simba, Seleman Matola amesema kutokana na kucheza mechi kila baada ya siku mbili watakuwa na mabadiliko katika kikosi chao kwani baadhi ya wachezaji wamepewa mapumziko.

Matola amesema hayo leo Machi 11,2024 wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maandalizi ya mchezo huo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, utakaochezwa kesho kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi.

“Kwa sababu ukingali ‘game’ zipo kila baada ya siku mbili kwa hiyo nafikiri  kunaweza kuwa na mabadiliko kutokana na kuwapa baadhi ya wachezaji mapumziko, sisi kama benchi la ufundi tutaangalia ni nani anaweza kutufaa katika mchezo wa kesho,” amesema Matola.

Aidha amesema morali yao ipo juu na bado wana nafasi kubwa ya kufanya vizuri katika ligi kuu na kuahidi kuwafurahisha mashabiki wa timu hiyo.

Amekiri kuwa walifanya makosa katika michezo miwili iliyopita dhidi ya Tanzania Prisons Coastal Union  kwa kuruhusu mabao lakini wameshajirekebisha mazoezini.

Katika mchezo uliopita Wekundu wa Msimbazi hao waliifunga Coastal Union 2-1 kwenye Uwanja wa Mkwakwani Tanga.

spot_img

Latest articles

VIJANA WAHAMASISHWA KUTUMIA FURSA ZA MADINI KUJIKWAMUA KIUCHUMI

Na Mwandishi Wetu VIJANA nchini wamehimizwa kutumia nguvu kazi, maarifa na ubunifu wao kuchangamkia...

TTCL yatumia Nanenane kuhamasisha matumizi ya huduma za Cloud

Na Mwandishi Wetu, Dodoma SHIRIKA la Mawasiliano Tanzania (TTCL), kupitia Kituo cha Taifa cha Kuhifadhi...

Bodi ya Chai yahamasisha matumizi ya chai kwa manufaa ya afya

Na Mwandishi Wetu, Dodoma BODI ya Chai Tanzania imewahamasisha Watanzania kujenga utamaduni wa kunywa chai...

NIRC kutekeleza miradi 30 ya umwagiliaji, kufungua maelfu ya ajira kwa vijana

Na Mwandishi Wetu, Dodoma SERIKALI kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC) imezindua mkakati wa...

More like this

VIJANA WAHAMASISHWA KUTUMIA FURSA ZA MADINI KUJIKWAMUA KIUCHUMI

Na Mwandishi Wetu VIJANA nchini wamehimizwa kutumia nguvu kazi, maarifa na ubunifu wao kuchangamkia...

TTCL yatumia Nanenane kuhamasisha matumizi ya huduma za Cloud

Na Mwandishi Wetu, Dodoma SHIRIKA la Mawasiliano Tanzania (TTCL), kupitia Kituo cha Taifa cha Kuhifadhi...

Bodi ya Chai yahamasisha matumizi ya chai kwa manufaa ya afya

Na Mwandishi Wetu, Dodoma BODI ya Chai Tanzania imewahamasisha Watanzania kujenga utamaduni wa kunywa chai...