Simba yaibadilishia kikosi Singida

Na Winfrida Mtoi

Kuelekea mechi yao na Singida Fountain Gate, Kocha Msaidizi wa Simba, Seleman Matola amesema kutokana na kucheza mechi kila baada ya siku mbili watakuwa na mabadiliko katika kikosi chao kwani baadhi ya wachezaji wamepewa mapumziko.

Matola amesema hayo leo Machi 11,2024 wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maandalizi ya mchezo huo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, utakaochezwa kesho kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi.

“Kwa sababu ukingali ‘game’ zipo kila baada ya siku mbili kwa hiyo nafikiri  kunaweza kuwa na mabadiliko kutokana na kuwapa baadhi ya wachezaji mapumziko, sisi kama benchi la ufundi tutaangalia ni nani anaweza kutufaa katika mchezo wa kesho,” amesema Matola.

Aidha amesema morali yao ipo juu na bado wana nafasi kubwa ya kufanya vizuri katika ligi kuu na kuahidi kuwafurahisha mashabiki wa timu hiyo.

Amekiri kuwa walifanya makosa katika michezo miwili iliyopita dhidi ya Tanzania Prisons Coastal Union  kwa kuruhusu mabao lakini wameshajirekebisha mazoezini.

Katika mchezo uliopita Wekundu wa Msimbazi hao waliifunga Coastal Union 2-1 kwenye Uwanja wa Mkwakwani Tanga.

spot_img

Latest articles

Viongozi Chadema washinda shauri la kuidharau Mahakama

Na Mwandishi Wetu Mahakama Kuu Masjala Ndogo Dar es Salaam imetupilia mbali shauri la maombi...

Ridhiwani:Niko tayari kuhojiwa kuhusu tuhuma za Lake Oil

Na Mwandishi Wetu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na...

Ndejembi: Ufanisi wa Tanesco katika utekelezaji na Usimamizi wa miradi umeleta mfumo madhubuti wa Nishati

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, amesema kuwa Shirika la Umeme...

Maboresho ya mitambo ya kufua umeme Mtera yaimarisha uzalishaji umeme

Na Mwandishi Wetu, Mtera NAIBU Waziri wa Nishati, Salome Makamba, Novemba 26, 2025, alitembelea na...

More like this

Viongozi Chadema washinda shauri la kuidharau Mahakama

Na Mwandishi Wetu Mahakama Kuu Masjala Ndogo Dar es Salaam imetupilia mbali shauri la maombi...

Ridhiwani:Niko tayari kuhojiwa kuhusu tuhuma za Lake Oil

Na Mwandishi Wetu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na...

Ndejembi: Ufanisi wa Tanesco katika utekelezaji na Usimamizi wa miradi umeleta mfumo madhubuti wa Nishati

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, amesema kuwa Shirika la Umeme...