Biden: Tendo la ndoa siri ya furaha kwenye ndoa

Rais Joe Biden wa Marekani amewaasa wasaidizi wake kwamba siri ya ndoa ya muda mrefu na ya kudumu ni “tendo la ndoa.” Kitabu kipya kuhusu mke wa rais, Jill Biden ambacho kinaangazia ndoa yao iliyodumu kwa miaka 47 sasa, kinalitaja ‘Tendo la ndoa’ kuwa ndio kirutubisho muhimu zaidi katika ndoa.

Kitabu hicho “American Woman – The Transformation of the Modern First Lady, from Hillary Clinton to Jill Biden,” kimeandikwa na mwandishi wa New York Times katika Ikulu ya White House, Katie Rogers na kinatarajiwa kutoka wiki hii.

Sehemu inayohusu ngono inachukua vifungu vichache tu katika kitabu hicho chenye kurasa 276, lakini tayari maudhui hayo yameibua mjadala mkubwa mitandaoni na kugonga vichwa vya habari sehemu mbalimbali duniani.

Jill Tracy Jacobs Biden, mke wa pili na wa sasa wa Biden, alizaliwa Juni 3, 1951. Alikutana na Biden Machi 1975. Kitabu hiki pia kinaelezea uchungu wa Biden alioupata baada ya mke wake wa kwanza, Neilia, kufariki katika ajali ya gari mwaka wa 1972 pamoja na binti yao Naomi.

Je unakubaliana na kauli hii ya rais Biden?

spot_img

Latest articles

Mhudumu wa mochwari mbaroni kwa tuhuma za kukutwa na viungo vya binadamu

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi mkoani Kagera linawashikilia watu wawili akiwamo mhudumu wa mochwari...

Katibu wa fedha UVCCM Dar arudisha fomu ya ridhaa ya ubunge Kawe

Katibu wa Uchumi, Mipango na Fedha UVCCM Mkoa wa Dar es Salaam, Hassan Ali...

Majaliwa  atangaza hagombei tena ubunge Ruangwa

Na Mwandishi Wetu Waziri mkuu na Mbunge wa Jimbo la Ruangwa, Kassim Majaliwa leo Julai...

Vijana, Dira na CCM. Chama pekee chenye Imani na vijanaTangu kuasisiwa

Na Mwandishi Wetu TANGU kuasisiwa kwake tarehe 5 Februari 1977 kwa muungano wa TANU...

More like this

Mhudumu wa mochwari mbaroni kwa tuhuma za kukutwa na viungo vya binadamu

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi mkoani Kagera linawashikilia watu wawili akiwamo mhudumu wa mochwari...

Katibu wa fedha UVCCM Dar arudisha fomu ya ridhaa ya ubunge Kawe

Katibu wa Uchumi, Mipango na Fedha UVCCM Mkoa wa Dar es Salaam, Hassan Ali...

Majaliwa  atangaza hagombei tena ubunge Ruangwa

Na Mwandishi Wetu Waziri mkuu na Mbunge wa Jimbo la Ruangwa, Kassim Majaliwa leo Julai...