Biden: Tendo la ndoa siri ya furaha kwenye ndoa

Rais Joe Biden wa Marekani amewaasa wasaidizi wake kwamba siri ya ndoa ya muda mrefu na ya kudumu ni “tendo la ndoa.” Kitabu kipya kuhusu mke wa rais, Jill Biden ambacho kinaangazia ndoa yao iliyodumu kwa miaka 47 sasa, kinalitaja ‘Tendo la ndoa’ kuwa ndio kirutubisho muhimu zaidi katika ndoa.

Kitabu hicho “American Woman – The Transformation of the Modern First Lady, from Hillary Clinton to Jill Biden,” kimeandikwa na mwandishi wa New York Times katika Ikulu ya White House, Katie Rogers na kinatarajiwa kutoka wiki hii.

Sehemu inayohusu ngono inachukua vifungu vichache tu katika kitabu hicho chenye kurasa 276, lakini tayari maudhui hayo yameibua mjadala mkubwa mitandaoni na kugonga vichwa vya habari sehemu mbalimbali duniani.

Jill Tracy Jacobs Biden, mke wa pili na wa sasa wa Biden, alizaliwa Juni 3, 1951. Alikutana na Biden Machi 1975. Kitabu hiki pia kinaelezea uchungu wa Biden alioupata baada ya mke wake wa kwanza, Neilia, kufariki katika ajali ya gari mwaka wa 1972 pamoja na binti yao Naomi.

Je unakubaliana na kauli hii ya rais Biden?

spot_img

Latest articles

Oktoba 29 siku ya giza, ifungue milango ya haki

OKTOBA 29, 2025 itabakia kuwa siku ya giza na machungu katika historia ya Jamhuri...

Fountain Gate yatoa kocha bora

Na Mwandishi Wetu Kocha wa timu ya Fountain Gate,  Mohamed Laizer amechaguliwa kuwa kocha bora...

Nyota JKT Queens aipigia hesabu Asec Mimosa

Na Winfrida Mtoi Mshambuliaji wa JKT Queens FC, Jamila Rajabu, amesema  amejipanga  kutengeneza  nafasi na...

Zungu achaguliwa kuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Na Mwandishi Wetu MBUNGE mteule wa Jimbo la Ilala Mussa Azzan Zungu ameibuka mshindi...

More like this

Oktoba 29 siku ya giza, ifungue milango ya haki

OKTOBA 29, 2025 itabakia kuwa siku ya giza na machungu katika historia ya Jamhuri...

Fountain Gate yatoa kocha bora

Na Mwandishi Wetu Kocha wa timu ya Fountain Gate,  Mohamed Laizer amechaguliwa kuwa kocha bora...

Nyota JKT Queens aipigia hesabu Asec Mimosa

Na Winfrida Mtoi Mshambuliaji wa JKT Queens FC, Jamila Rajabu, amesema  amejipanga  kutengeneza  nafasi na...