Watanzania washinda milioni 234 za AGT, Rais Samia awapongeza


Na Mwandishi wetu

Wanasarakasi wawili watanzania ambao ni ndugu, Fadhil Ramadhani na Ibrahim Job, wameshinda kitita cha fedha cha dola za Kimarekani 250,000 sawa na sh 634 milioni baada ya kuibuka washindi wa American Got Talent (AGT) Fantasy League.

Watanzania hao wanaounda kikundi cha sarakasi kinachoitwa Ramadhani  Brothers, waliibuka washindi usiku wa jana Februari 19,2024 kwa kuwashinda wapinzani wao wengine tisa waliofika nao fainali.

Kupitia ukurasa wao wa Instagram baada ya kutangazwa washindi katika usiku huo, wamesema ni ushindi wa kushangaza kwao na kuwashukuru wote waliowapa sapoti.

Wamesema wanajivunia  kutangazwa wabingwa wa dunia wa mashindano, huku wakiwapokeza washindani wenzao  ambao wamewafanya wawe bora zaidi.

Katika hatua nyingine Rais Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza washindi hao kutokana na kuitangaza vema Tanzania.

“Pongezi kwa vijana wetu Fadhil na Ibrahim (The Ramadhan Brothers) kwa kuibuka washindi katika mashindano ya sanaa na burudani ya AGT: Fantasy League, safari yenu inaendelea kudhihirisha kuwa juhudi, nidhamu, kujituma na kujiamini ni nguzo muhimu kufikia mafanikio. Mnaitangaza vyema nchi yetu na kuweka mfano bora kwa wengine,” amesema Rais Samia.

spot_img

Latest articles

Ndumbaro: Sheria 300 Zimetafsiriwa kwa Kiswahili Ili Kuimarisha Uelewa kwa Wananchi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Katiba na Sheria, Dkt. Damas Ndumbaro, amesema kuwa hadi...

Jessica: CCM inajali uongozi wa vijana

Na Mwandishi Wetu KATIBU wa Idara ya Uhamasishaji na Chipukizi UVCCM TAIFA, Jessica Mshama...

Waziri Aweso: Tuna uhakika wa maji ya kutosha Dar na Pwani

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso amewatoa hofu wakazi wa mikoa ya...

PURA yajivunia mafanikio katika Ajenda ya Nishati Safi na ushiriki wa Watanzania Sekta ya Mafuta na Gesi

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Kudhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) imesema inajivunia...

More like this

Ndumbaro: Sheria 300 Zimetafsiriwa kwa Kiswahili Ili Kuimarisha Uelewa kwa Wananchi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Katiba na Sheria, Dkt. Damas Ndumbaro, amesema kuwa hadi...

Jessica: CCM inajali uongozi wa vijana

Na Mwandishi Wetu KATIBU wa Idara ya Uhamasishaji na Chipukizi UVCCM TAIFA, Jessica Mshama...

Waziri Aweso: Tuna uhakika wa maji ya kutosha Dar na Pwani

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso amewatoa hofu wakazi wa mikoa ya...