Papa Francis akutana na Rais Samia

Baba Mtakatifu Francisko amekutana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan huku wakieleza dhamira yao ya pamoja ya kuhimiza amani duniani.

Baba Mtakatifu Francisko amempokea Rais Samia na ujumbe, mjini Vatican siku ya Jumatatu. Baada ya kukutana na Baba Mtakatifu Francisko, Rais amekutana na Katibu wa Jimbo la Vatican, Kardinali Pietro Parolin, akifuatana na Katibu wa Vatican anayeshughulikia Mahusiano na Mataifa na Mashirika ya Kimataifa, Askofu Mkuu, Paul Richard Gallagher.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ofisi Rasmi ya Mawasiliano ya Vatican (Holy See Press Office), viongozi hao wawili walikuwa na mjadala mzuri ambao pamoja na mambo mengine umeangazia uhusiano mwema uliopo kati ya Tanzania na Vatican.

Kadhalika wamezungumzia “mchango muhimu ambao Kanisa Katoliki limekuwa likitoa nchini Tanzania hasa katika sekta za elimu na afya. Kadhalika wamezungumzia hali ya kikanda na mambo ya sasa ya kimataifa, na pande zote mbili zilielezea matakwa yao ya pamoja ya kuhimiza amani.

Chanzo: Vatican Radio

spot_img

Latest articles

Tumeepuka balaa jingine, uadilifu uongoze tiba machungu ya MO29

JUMANNE wiki hii Watanzania walisherehekea siku ya uhuru wa Tanganyika wengi wakiwa majumbani kwao....

Aweso aridhishwa na wingi wa maji Ruvu Juu, aipa Dawasa jukumu

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa maji, Jumaa Aweso amekagua na kujiridhisha na wingi wa...

Prof. Mkenda: Serikali imeendelea kufanya mageuzi makubwa katika sekta ya Elimu

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, amesema Serikali...

Jeshi la Polisi latoa onyo wanaondelea kuhamasisha maandamano

Na Mwandishi Wetu JESHI la Polisi nchini limesema  kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi...

More like this

Tumeepuka balaa jingine, uadilifu uongoze tiba machungu ya MO29

JUMANNE wiki hii Watanzania walisherehekea siku ya uhuru wa Tanganyika wengi wakiwa majumbani kwao....

Aweso aridhishwa na wingi wa maji Ruvu Juu, aipa Dawasa jukumu

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa maji, Jumaa Aweso amekagua na kujiridhisha na wingi wa...

Prof. Mkenda: Serikali imeendelea kufanya mageuzi makubwa katika sekta ya Elimu

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, amesema Serikali...