Papa Francis akutana na Rais Samia

Baba Mtakatifu Francisko amekutana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan huku wakieleza dhamira yao ya pamoja ya kuhimiza amani duniani.

Baba Mtakatifu Francisko amempokea Rais Samia na ujumbe, mjini Vatican siku ya Jumatatu. Baada ya kukutana na Baba Mtakatifu Francisko, Rais amekutana na Katibu wa Jimbo la Vatican, Kardinali Pietro Parolin, akifuatana na Katibu wa Vatican anayeshughulikia Mahusiano na Mataifa na Mashirika ya Kimataifa, Askofu Mkuu, Paul Richard Gallagher.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ofisi Rasmi ya Mawasiliano ya Vatican (Holy See Press Office), viongozi hao wawili walikuwa na mjadala mzuri ambao pamoja na mambo mengine umeangazia uhusiano mwema uliopo kati ya Tanzania na Vatican.

Kadhalika wamezungumzia “mchango muhimu ambao Kanisa Katoliki limekuwa likitoa nchini Tanzania hasa katika sekta za elimu na afya. Kadhalika wamezungumzia hali ya kikanda na mambo ya sasa ya kimataifa, na pande zote mbili zilielezea matakwa yao ya pamoja ya kuhimiza amani.

Chanzo: Vatican Radio

spot_img

Latest articles

Waziri Mkuu atoa sababu yakutotaja idadi vifo vilivyotokea Oktoba 29

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amesema ni muhimu watanzania kutanguliza utu na...

Niffer arudishwa gerezani, 20 kesi ya uhaini waachiwa huru

Na Mwandishi Wetu Watuhumiwa 20 kati ya 22 waliokuwa wanashtakiwa kwa makosa ya uhaini wameachiwa...

Dk.Mwigulu aagiza Kanisa Gwajima lifunguliwe

Na Mwandishi Wetu Waziri Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba ameagiza kufunguliwa kwa Kanisa la Ufufuo na...

Ndejembi asisitiza ushirikiano kwa viongozi katika utekelezaji wa miradi yenye kipaumbele kwa wananchi

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi (Mb), ametoa wito kwa viongozi na...

More like this

Waziri Mkuu atoa sababu yakutotaja idadi vifo vilivyotokea Oktoba 29

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amesema ni muhimu watanzania kutanguliza utu na...

Niffer arudishwa gerezani, 20 kesi ya uhaini waachiwa huru

Na Mwandishi Wetu Watuhumiwa 20 kati ya 22 waliokuwa wanashtakiwa kwa makosa ya uhaini wameachiwa...

Dk.Mwigulu aagiza Kanisa Gwajima lifunguliwe

Na Mwandishi Wetu Waziri Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba ameagiza kufunguliwa kwa Kanisa la Ufufuo na...