Papa Francis akutana na Rais Samia

Baba Mtakatifu Francisko amekutana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan huku wakieleza dhamira yao ya pamoja ya kuhimiza amani duniani.

Baba Mtakatifu Francisko amempokea Rais Samia na ujumbe, mjini Vatican siku ya Jumatatu. Baada ya kukutana na Baba Mtakatifu Francisko, Rais amekutana na Katibu wa Jimbo la Vatican, Kardinali Pietro Parolin, akifuatana na Katibu wa Vatican anayeshughulikia Mahusiano na Mataifa na Mashirika ya Kimataifa, Askofu Mkuu, Paul Richard Gallagher.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ofisi Rasmi ya Mawasiliano ya Vatican (Holy See Press Office), viongozi hao wawili walikuwa na mjadala mzuri ambao pamoja na mambo mengine umeangazia uhusiano mwema uliopo kati ya Tanzania na Vatican.

Kadhalika wamezungumzia “mchango muhimu ambao Kanisa Katoliki limekuwa likitoa nchini Tanzania hasa katika sekta za elimu na afya. Kadhalika wamezungumzia hali ya kikanda na mambo ya sasa ya kimataifa, na pande zote mbili zilielezea matakwa yao ya pamoja ya kuhimiza amani.

Chanzo: Vatican Radio

spot_img

Latest articles

Simba yaachia pointi tatu kwa Mkapa, Azam nayo mambo magumu

Na Winfrida Mtoi Simba imeshindwa kutamba nyumbani baada ya kufungwa na Petro de Luanda bao...

Serikali yaahidi kushirikiana na wadau kuendeleza mchezo wa kuogelea

Na Winfrida Mtoi WADAU wa mchezo wakuogelea Afrika Mashariki wamekutana kujadili maendeleo ya mchezo huo,...

Ndejembi: Tanesco mmefanya mageuzi makubwa katika huduma ya umeme kwa wananchi

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amesema kuwa Shirika la Umeme Tanzania...

Dube awapa raha wananchi

Na Winfrida Mtoi BAO pekee lililofungwa na Prince Dube dakika ya 58, limeipa Yanga alama...

More like this

Simba yaachia pointi tatu kwa Mkapa, Azam nayo mambo magumu

Na Winfrida Mtoi Simba imeshindwa kutamba nyumbani baada ya kufungwa na Petro de Luanda bao...

Serikali yaahidi kushirikiana na wadau kuendeleza mchezo wa kuogelea

Na Winfrida Mtoi WADAU wa mchezo wakuogelea Afrika Mashariki wamekutana kujadili maendeleo ya mchezo huo,...

Ndejembi: Tanesco mmefanya mageuzi makubwa katika huduma ya umeme kwa wananchi

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amesema kuwa Shirika la Umeme Tanzania...