Safari za ndege Poland hadi Tanzania kuanza

Na Esther Mnyika

Rais Dk. Samia Suluhu Hassan ametoa maelekezo ya kuanzisha safari za ndege za moja kwa moja kutoka Poland hadi Tanzania.

Akizungumza leo Februari 9, 2024 Ikulu, jijini Dar es Salaam na waandishi wa habari baada mazungumzo na Rais wa Poland, Andrzej Duda, Rais Samia amesema ziara ya rais huyo nchini ni fursa ya kuimarisha uhusiano zaidi wa nchi hizo mbili.

Amesema ziara hiyo ni kilelezo kuimarisha uhusiano ulioanza mwaka 1962 ikiwa umetimiza miaka 62.

“Ili kuchochea zaidi utalii na biashara hapa nchini wataalamu wameelekezwa kuchukua hatua zitakazo wezesha kuanza safari za ndege kutoka Poland hadi Tanzania moja kwa moja, tumeweka ombi letu kwa ukubwa nchini Poland, “amesema Dk. Samia.

Amesema Poland ni miongoni mwa nchi 10 ambazo raia wake wengi hutembelea Tanzania kwa shughuli za utalii.

Amesema takwimu zinaonyesha watalii kutoka Poland mwaka 2023 walikuwa 41000 na ndani ya mwezi mmoja mwaka huu wamekuja 6000.

Amesema wamekubaliana na Rais huyo kuimarisha ushirikiano uliopo na kuhamasisha uwekezaji zaidi kwenye sekta za mikakati kama vile viwanda, madini gesi asilia na uchumi wa buluu.

“Tumeendelea uhusiano kati ya Tanzania na Poland katika sekta mbalimbali ikiwemo kilimo, elimu, uwekezaji, utalii, viwanda, uchumi wa buluu na TEHAMA,”amesema.

Aidha amewakaribisha wawekezaji hususani wa utalii kuwekeza katika ujenzi hoteli nchini kwa kuwa kuna maeneo mazuri ya uwekezaji katika uzalishaji.

Naye Rais wa Poland, Duda amesema ziara yake nchini imelenga kuibua maeneo mapya ya ushirikiano kati ya nchi hizo mbili na kuleta faida mbeleni.

Amesema wamekuwa na uhusiano wa miaka 62 na Tanzania na kuimarisha uhusiano wao tangu vita ya pili ya dunia.

“Nitaimarisha uhusiano katika sekta ya utalii na watalii kuendelea kuongezeka kuja kutembelea Tanzania na kushawishi wawekezaji kuja kuwekeza Tanzania kutoka Poland,”amesema Rais Duda.

Amesema kuimarisha sekta ya elimu, biashara na uchumi ikiwemo wanafunzi kutoka Tanzania kwenda kusoma Poland katika vyuo mbalimbali kwa ufadhili nchi hiyo.

“Vijana watafaidika kusoma katika vyuo hivi watajifunza mambo mbalimbali ikiwemo mabadiliko ya Tabia Nchi na TEHAMA, watapata ujuzi wa kutunza vitu hivi,”amesema.

Aidha amewalika Rais Dk.Samia nchini Poland ikiwa ni fursa ya kutaanda jukwaa la kuwakutanisha wawekezaji nchini humo kujadili fursa za uwekezaji.

spot_img

Latest articles

Tanzania Kunufaika na Mradi wa Umoja wa Ulaya wa Kukabiliana na Hatari za Sumu za Kemikali

Na Mwandishi wetu TANZANIA iko katika hatua za awali za upembuzi wa kushiriki katika mradi...

Rostam Aziz ainunua Nation Media ya Kenya

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI ya Taarifa Limited inayomilikiwa na mfanyabiashara Rostam Aziz imeingia makubaliano ya...

Mwili wa Mwanahabari Mkongwe Makaranga waagwa Dar, kuzikwa Mwanza

Na Mwandishi Wetu WAANDISHI wa Habari, Wahariri, ndugu na jamaa leo Machi 10, 2026, wamejumuika...

Wanawake TRA Wapongezwa kwa Mchango wa Ukusanyaji Mapato

Na Mwandishi Wetu KATIBU Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dkt. Natu Mwamba, amewapongeza wanawake wa...

More like this

Tanzania Kunufaika na Mradi wa Umoja wa Ulaya wa Kukabiliana na Hatari za Sumu za Kemikali

Na Mwandishi wetu TANZANIA iko katika hatua za awali za upembuzi wa kushiriki katika mradi...

Rostam Aziz ainunua Nation Media ya Kenya

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI ya Taarifa Limited inayomilikiwa na mfanyabiashara Rostam Aziz imeingia makubaliano ya...

Mwili wa Mwanahabari Mkongwe Makaranga waagwa Dar, kuzikwa Mwanza

Na Mwandishi Wetu WAANDISHI wa Habari, Wahariri, ndugu na jamaa leo Machi 10, 2026, wamejumuika...