Waitara Trophy kutimua vumbi Lugalo

Na Winfrida Mtoi

Shindano la Gofu la kumuenzi aliyekuwa Mkuu wa Majeshi Jenerali Mstaafu, George Waitara ‘NBC Waitara Trophy 2024’ litarajia kufanyika Jumamosi Januari 27,2024 ambapo zaidi wachezaji 100 watachuana kwenye viwanja vya Klabu ya Gofu Lugalo, jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi habari leo Januari 25,2024 jijini Dar es Salaam, Meneja wa Klabu ya Gofu Lugalo, Kanali David Mzaray amesema shindano hilo ni la wazi kila mtu anaruhusiwa kushiriki.

Amesema katika shindano hilo la kumuenzi muasisi huyo wa Klabu ya Gofu Lugalo, wamealika klabu zote za gofu nchini na hadi kufikia leo wachezaji waliokuwa wamejisajili ni 118.

Ameeleza kuwa idadi hiyo ya wachezaji inatarajiwa kuongezeka kutokana na kasi ya usajili inayoendelea na lengo ni kufikia washiriki 200.

“Shindano hili ni la siku moja na ni la wazi mtu yoyote anaruhusiwa kushiriki kutoka ndani na nje ya nchi. Litashirikisha wachezaji wa division zote, A, B,C, seniors, juniors na ladies na zawani ni kwa washindi wote,”amefafanua Mziray.

Naye Mkuu wa Masoko wa Benki ya NBC ambao ni wadhamini wakuu wa shindano hilo, David Raymond amesema ni furaha kwao kuona shindano hilo linazidi kukua kila mwaka.

Amesema huu ni mwaka wa nne wanadhamini na wanajivunia kuona mafanikio ya shindano hilo kwani hata wao wana timu inashiriki.

Kwa upande wake Mkuu wa Uhusiano wa SBC, Foti Nyirenda amesema wamedhamini shindano hilo ili kuendeleza ndoto za muasisi huyo klabu ya Lugalo katika kukuza mchezo wa gofu.

spot_img

Latest articles

NEMC yatoa elimu kwa umma kuelekea kilele cha Siku ya Kimataifa ya Taka Sifuri

Na Tatu Mohamed BARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeanza kutoa...

Vijana 521 waondoka kwa ajira nje ya nchi

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imewaaga vijana 521 waliopata fursa za ajira nje ya nchi, hatua...

Naibu Waziri wa Nishati akabidhi vitendea kazi Kwa Tanesco Mkoa wa Shinyanga

📌Ni katika muendelezo wa mkakati wa shirika wa kuwahudumia wananchi kwa ufanisi 📌Awasihi wananchi kutumia...

Matendo ya Polisi ni hujuma dhidi ya utawala bora, demokrasia

MFUMO wa uchumi wa soko huru una kanuni zake. Miongoni mwake ni kuruhusu ushindani....

More like this

NEMC yatoa elimu kwa umma kuelekea kilele cha Siku ya Kimataifa ya Taka Sifuri

Na Tatu Mohamed BARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeanza kutoa...

Vijana 521 waondoka kwa ajira nje ya nchi

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imewaaga vijana 521 waliopata fursa za ajira nje ya nchi, hatua...

Naibu Waziri wa Nishati akabidhi vitendea kazi Kwa Tanesco Mkoa wa Shinyanga

📌Ni katika muendelezo wa mkakati wa shirika wa kuwahudumia wananchi kwa ufanisi 📌Awasihi wananchi kutumia...