Isha Mashauzi aibukia Mtata Mtatuzi

Na Winfrida Mtoi

Mwanamuziki wa miondoko ya taarabu, Isha Mashauzi atakuwa miongoni mwa watakaoshudia a pambano la ngumi la bondia Hassan Mwakinyo lililopewa jina la Mtata Mtatuzi.

Mwakinyo anatarajiwa kupanda ulingoni Januari 27, 2024 kuzichapa na Mbiya Kanku raia wa DR Congo pambano la ubingwa wa WBO Afrika litakalopigwa Amani Complex Indoor Arena, Zanzibar.

Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kuelekea visiwani humo, Isha amesema alikuwepo Ubungo Plaza Desemba 26, 2023 na kushudia vitasa hasa kwa wanawake hivyo kuamua kwenda tena Zanzibar kuona burudani hiyo.

Ameeleza kuwa lengo ni kupeana sapoti kwa sababu ngumi na muziki vyote vinakwenda pamoja.

“Ngumi ni muziki na muziki ni ngumi. Zamani tulikuwa tunaamini kwamba wanaopenda michezo hii ni wanaume tu na ni hatari lakini sasa hivj hata watoto wa kike wanafanya vizuri ndiyo maana nikaamua kuja kusapoti,” amesema Isha.

Amesema kwa hali ilivyo Tanzania itafika mbali kupitia mchezo wa ngumi, huku akiwataka mashabiki kununua tiketi ili kushuhudia mapambano hayo.

Kwa upande wake Mwakinyo amesema ameshakamilisha maandalizi na kutamba kuwa yeye ni bondia mkubwa hana mpinzani nchini.

spot_img

Latest articles

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

Serikali: Tuchukue hatua kuepuka madhara ya usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa (UVIDA)

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia kwa Mkurugenzi msaidizi, Kitengo cha Afya Moja, Ofisi ya...

Serikali yawaita wadau kujitokeza kusapoti ushiriki wa wanawake michezoni

Na Winfrida Mtoi Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma 'MwanaFA' amewaomba...

Ndejembi awahakikishia wakazi wa Kigamboni umeme wa uhakika

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amefanya ziara ya kikazi ndani ya...

More like this

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

Serikali: Tuchukue hatua kuepuka madhara ya usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa (UVIDA)

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia kwa Mkurugenzi msaidizi, Kitengo cha Afya Moja, Ofisi ya...

Serikali yawaita wadau kujitokeza kusapoti ushiriki wa wanawake michezoni

Na Winfrida Mtoi Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma 'MwanaFA' amewaomba...