Mwakinyo atamba yuko fiti asilimia 98 kupanda ulingoni Zanzibar

Na Winfrida Mtoi

Zikiwa zimebaki siku chache kabla ya pambano lake dhidi ya Mbiya Kanku litakalofanyika Januari 27, 2024, bondia wa Hassan Mwakinyo amesema amekamilisha maandalizi kwa asilimia 98 kilichobaki ni kupima uzito pekee.

Mwakinyo na Kanku raia wa DR Congo wanatarajiwa kupanda ulingoni katika pambano la ubingwa wa WBO Afrika litakalopigwa Amani Complex Indoor Arena, Zanzibar.

Mwakinyo amesema amejiandaa kila idara, hivyo mpizani hata akimjia kwa mtindo gani yupo tayari kupambana naye, kwani mikono ndiyo itaongea ulingoni.

Bondia huyo mwenye jina kubwa nchini, amewatoa hofu mashabiki wa masumbwi visiwani Zanzibar na Tanzania kwa ujumla kuwa siku hiyo ataonesha burudani ya kuvutia ya ngumi.

Mapambano mengine yatakayopigwa siku hiyo, Hussein Itaba dhidi ya Juma Misumari wa Morogoro, Bakari H.Bakari na Seleman Hamad, Masoud Khatibu atazichapa na Yahaya Khamis, huku mwanadada Zulfa Iddi akivaana na Debora Mwenda.

spot_img

Latest articles

Dkt Biteko: Serikali kuendelea kuwekeza katika sekta ya Afya

📌 Dkt. Biteko atambelea Hospitali ya Wilaya ya Meru Na Mwandishi Wetu SERIKALI imeahidi kuendelea...

THRDC yashauri kuitishwa mkutano wa kitaifa wa maridhiano

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC)...

Sh. Bilioni 30 zaidhinishwa kujenga Barabara zilizoathiriwa na mvua

Na Mwandishi Wetu SERIKALI ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imepanga kutumia kiasi cha...

Ewura yazitaka kampuni za gesi kuongeza mawakala, kudhibiti uchakachuaji wa gesi

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam MAMLAKA ya Udhibiti wa Huduma za nishati na...

More like this

Dkt Biteko: Serikali kuendelea kuwekeza katika sekta ya Afya

📌 Dkt. Biteko atambelea Hospitali ya Wilaya ya Meru Na Mwandishi Wetu SERIKALI imeahidi kuendelea...

THRDC yashauri kuitishwa mkutano wa kitaifa wa maridhiano

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC)...

Sh. Bilioni 30 zaidhinishwa kujenga Barabara zilizoathiriwa na mvua

Na Mwandishi Wetu SERIKALI ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imepanga kutumia kiasi cha...