Mwakinyo atamba yuko fiti asilimia 98 kupanda ulingoni Zanzibar

Na Winfrida Mtoi

Zikiwa zimebaki siku chache kabla ya pambano lake dhidi ya Mbiya Kanku litakalofanyika Januari 27, 2024, bondia wa Hassan Mwakinyo amesema amekamilisha maandalizi kwa asilimia 98 kilichobaki ni kupima uzito pekee.

Mwakinyo na Kanku raia wa DR Congo wanatarajiwa kupanda ulingoni katika pambano la ubingwa wa WBO Afrika litakalopigwa Amani Complex Indoor Arena, Zanzibar.

Mwakinyo amesema amejiandaa kila idara, hivyo mpizani hata akimjia kwa mtindo gani yupo tayari kupambana naye, kwani mikono ndiyo itaongea ulingoni.

Bondia huyo mwenye jina kubwa nchini, amewatoa hofu mashabiki wa masumbwi visiwani Zanzibar na Tanzania kwa ujumla kuwa siku hiyo ataonesha burudani ya kuvutia ya ngumi.

Mapambano mengine yatakayopigwa siku hiyo, Hussein Itaba dhidi ya Juma Misumari wa Morogoro, Bakari H.Bakari na Seleman Hamad, Masoud Khatibu atazichapa na Yahaya Khamis, huku mwanadada Zulfa Iddi akivaana na Debora Mwenda.

spot_img

Latest articles

Safari ya ‘TLP’ ya Lissu ni ipi?

MWAKA 1992 wakati nchi hii ilipoingia katika mfumo wa vyama vingi vya siasa, kulikuwa...

Karibu 2025, tuyakatae magenge haya sasa

LEO ni siku ya pili katika mwaka mpya wa 2025. Ninawatakia wasomaji wa safu...

Kuubeba uozo wa 2024  kuingia 2025 ni fedheha

NI siku nne tu zimebakia kuupa kisogo mwaka 2024. Mwaka huu ulikuwa na mambo...

Hivi vikosi kazi vimerejea kwa mlango wa nyuma?

KUNA kila dalili kwamba taifa letu kidogokidogo linakumbwa na hali ya kutokuaminiana. Hali hii...

More like this

Safari ya ‘TLP’ ya Lissu ni ipi?

MWAKA 1992 wakati nchi hii ilipoingia katika mfumo wa vyama vingi vya siasa, kulikuwa...

Karibu 2025, tuyakatae magenge haya sasa

LEO ni siku ya pili katika mwaka mpya wa 2025. Ninawatakia wasomaji wa safu...

Kuubeba uozo wa 2024  kuingia 2025 ni fedheha

NI siku nne tu zimebakia kuupa kisogo mwaka 2024. Mwaka huu ulikuwa na mambo...