Watalii zaidi ya 2,000 watua nchini na meli ya Kitalii

Na Shani Nicolaus, Media Brains

Meli kubwa iliyobeba watalii 2,210 kutoka Canada, imewasili alfajiri ya leo Jumanne Januari 16, 2024 katika Bandari ya Dar es Salaam.

Meli hiyo maarufu kama Norwegian Cruise Line Dawn yenye urefu wa mita 294, imetajwa kuwa kubwa zaidi kuwasili katika bandari zote nchini Tanzania tangu kuanzishwa kwake.

Mkurugenzi wa Bandari ya Dar es Salaam, Mrisho Mrisho amewaambia wanahabari mapema leo kuwa hadi inafika Tanzania, meli hiyo imepitia katika bandari tofauti ikiwemo ile ya Mombasa, nchini Kenya na ina uwezo wa kubeba abiria 4,700, japo waliowasili ni watalii 2,210 pamoja na wafanyakazi zaidi ya 1,000.

Norwegian Cruise Line Dawn ilianza kufanya kazi mwaka 2002 ikiwa na thamani ya zaidi ya Sh trilioni 1, ina kimo cha mita 59, ikienda kwa kasi ya kilomita 46 kwa saa na ina wafanyakazi zaidi ya 1,000.

Rekodi zinaonyesha kuwa mara ya mwisho kwa meli ya kitalii kutia nanga katika Bandari ya Dar es Salaam, ilikuwa Novemba 10, 2022, ambapo meli ya Zaandam inayomilikiwa na Kampuni ya Holland American Line ilitia nanga kwa siku mbili kabla ya kuelekea visiwani Zanzibar, ikiwa na watalii 1,500.

Aidha, Aprili 8, 2022 Bandari ya Dar es Salaam ilipokea meli kubwa aina ya Frontier Ace iliyobeba magari 4,041 ikiwa ni ya kwanza kubeba mzigo mkubwa wa magari tangu kuanzishwa kwa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA).

Upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Damas Mfugale amesema watalii waliokuja na meli hiyo watatembelea mji wa kihistoria ya Bagamoyo, wengine watakwenda Hifadhi ya Selous kwa ajili ya kutazama wanyama na wengine watafanya utalii katika jiji la Dar es Salaam.

“Hii ni hatua ya muhimu kwenye uchumi wa utalii, tunatarajia kila watakapo pita Watanzania watanufaika,” amesema Mfugale.

Sehemu ya watalii hao waliokuja na meli hiyo, Suzanne Ramage na Gem Cheesman kutokana Canada, wamesema wanafuraha kufika Tanzania ikiwa ni mara yao ya kwanza.

spot_img

Latest articles

Yanga yatinga makundi CAFCL kibabe

Na Winfrida Mtoi Yanga imefanikiwa kutinga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL)...

Viongozi wa dini Kanda ya Kati wataka amani uchaguzi mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dodoma VIONGOZI wa dini mbalimbali kutoka Kanda ya Kati wamewataka Watanzania...

Viongozi wa dini Kanda ya Magharibi waazimia kudumisha amani kuelekea Uchaguzi Mkuu

Na Mwandishi Wetu, Tabora VIONGOZI wa dini katika mikoa ya Kanda ya Magharibi wameazimia...

Viongozi wa Dini Kanda ya Kusini wataka ulinzi amani, kujitokeza upigaji kura

Na Mwandishi Wetu, Lindi VIONGOZI wa dini mbalimbali kutoka mikoa ya Kanda ya Kusini wamewataka...

More like this

Yanga yatinga makundi CAFCL kibabe

Na Winfrida Mtoi Yanga imefanikiwa kutinga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL)...

Viongozi wa dini Kanda ya Kati wataka amani uchaguzi mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dodoma VIONGOZI wa dini mbalimbali kutoka Kanda ya Kati wamewataka Watanzania...

Viongozi wa dini Kanda ya Magharibi waazimia kudumisha amani kuelekea Uchaguzi Mkuu

Na Mwandishi Wetu, Tabora VIONGOZI wa dini katika mikoa ya Kanda ya Magharibi wameazimia...