Ramaphosa aafiki makubaliano ya Israel na Hamas

Johannesburg, Afrika Kusini

Rais wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa ameafiki makubaliano kati ya Israel na Hamas kuhusu usitishaji wa mapigano kwa siku nne. Usitishaji wa mapigano utakuwa ndani ya saa 24.

Cyril Ramaphosa ni mfuasi mkubwa wa Wapalestina

Kama sehemu ya mpango huo, Hamas itawaachilia huru mateka 50 iliowakamata mwezi uliopita na Israel itawaachilia wafungwa wapatao 150 wa Kipalestina.

Katika taarifa yake, Ramaphosa ameema: “Kama mwanachama wa Jumuiya ya Kimataifa inayotetea amani, haki na utawala wa sheria za kimataifa katika sehemu zote za dunia, Afrika Kusini inaafiki makubaliano yaliyofikiwa.

“Ni matumaini yangu kwamba kufikiwa kwa usitishaji huu wa mapigano kutaimarisha juhudi za kufikia mwisho wa moja kwa moja wa mzozo uliopo,” amesema kiongozi huyo wa Afrika Kusini.

Ikumbukzwe kuwa, Serikali ya Afrika Kusini – inayoongozwa na African National Congress (ANC) – ni mshirika wa muda mrefu wa Wapalestina.

Aidha, imeitaka Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) kutoa hati ya kukamatwa kwa Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu ifikapo katikati ya mwezi Disemba kutokana na operesheni ya kijeshi ya Israel katika Gaza.

Ilianzisha operesheni kubwa ya kijeshi mjini Gaza kujibu shambulio la kuvuka mpaka la Hamas Oktoba 7, ambapo watu wasiopungua 1,200 waliuawa na wengine zaidi ya 200 kuchukuliwa mateka.

Wizara ya afya ya Gaza inayoendeshwa na Hamas imesema takriban watu 14,000 wameuawa katika eneo hilo tangu Israel ilipoanzisha kampeni yake ya kulipiza kisasi.

spot_img

Latest articles

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

Viongozi wa dini waendelea kihimiza amani uchaguzi mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam VIONGOZI wa dini nchini wameendelea kuhimiza umuhimu wa kudumisha...

Ujumbe wa viongozi wa dini kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 29, 2025 katika Kongamano la Kamati ya Amani Kitaifa Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu Askofu Mkuu Wapo Mission, Dk. Sylvester Gamanywa “Mungu ambaye tunamwakilisha ndiye anayweka watawala...

Watumishi wa umma waaswa kushiriki Uchaguzi wa Oktoba 29

Dar es Salaam. Ofisi ya Msajili wa Hazina (OMH) imetoa wito kwa watumishi wote...

More like this

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

Viongozi wa dini waendelea kihimiza amani uchaguzi mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam VIONGOZI wa dini nchini wameendelea kuhimiza umuhimu wa kudumisha...

Ujumbe wa viongozi wa dini kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 29, 2025 katika Kongamano la Kamati ya Amani Kitaifa Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu Askofu Mkuu Wapo Mission, Dk. Sylvester Gamanywa “Mungu ambaye tunamwakilisha ndiye anayweka watawala...