Mahakama ya Kenya yaongeza muda wa amri ya kuzuia kutumwa kwa polisi nchini Haiti

Nairobi, Kenyad

Mahakama Kuu ya Kenya imeongeza muda wa amri ya kuzuia kutumwa kwa polisi hadi Haiti au nchi nyingine yoyote ikisubiri kusikilizwa zaidi.

Mapema mwezi huu mahakama ilisema walalamishi hao wameibua masuala muhimu ya kitaifa na maslahi ya umma.

Kenya ilikuwa imejitolea kuongoza kikosi cha kimataifa kwenda Haiti kusaidia kukomesha ghasia za magenge. Pia iliahidi kupeleka maafisa wake 1000 kwa misheni hiyo.

Ekuru Aukot aliyekuwa mgombeaji urais na mmoja wa walalamishi alisema katiba hailengi kutumwa kwa polisi nje ya nchi.

Aliongeza kuwa atalishtaki Baraza la Mawaziri kwa kudharau mahakama baada ya wao kuidhinisha kutumwa licha ya agizo la mahakama.

Bunge litahitaji kuidhinisha idhini hiyo kabla ya kuanza kutumwa.

Hata hivyo, timu ya wanasheria wanaowakilisha bunge la kitaifa iliambia mahakama kwamba bunge hilo haliwezi kujadili suala hilo hadi maagizo yatakapoondolewa.

Haiti imekumbwa na ghasia za magenge kwa miezi kadhaa. Kumekuwa na visa 3,000 vya mauaji na visa 1,500 vya utekaji nyara kwa ajili ya fidia kulingana na Umoja wa Mataifa.

Waziri Mkuu Ariel Henry alikuwa ametoa wito wa usaidizi wa kimataifa akisema serikali imezidiwa nguvu.

spot_img

Latest articles

Ndejembi: Ufanisi wa Tanesco katika utekelezaji na Usimamizi wa miradi umeleta mfumo madhubuti wa Nishati

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, amesema kuwa Shirika la Umeme...

Maboresho ya mitambo ya kufua umeme Mtera yaimarisha uzalishaji umeme

Na Mwandishi Wetu, Mtera NAIBU Waziri wa Nishati, Salome Makamba, Novemba 26, 2025, alitembelea na...

Ndejembi: Tanzania sasa ina umeme wa kutosha

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amesema Tanzania kwa sasa ina umeme...

Jeshi la Polisi lachunguza  taarifa ya OCD  Chunya

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi limesema limeona na linafanyia uchunguzi taarifa inayosambaa kwenye mitandao...

More like this

Ndejembi: Ufanisi wa Tanesco katika utekelezaji na Usimamizi wa miradi umeleta mfumo madhubuti wa Nishati

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, amesema kuwa Shirika la Umeme...

Maboresho ya mitambo ya kufua umeme Mtera yaimarisha uzalishaji umeme

Na Mwandishi Wetu, Mtera NAIBU Waziri wa Nishati, Salome Makamba, Novemba 26, 2025, alitembelea na...

Ndejembi: Tanzania sasa ina umeme wa kutosha

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amesema Tanzania kwa sasa ina umeme...