Warning: Array to string conversion in /home/themedia/domains/themediabrains.com/public_html/wp-includes/shortcodes.php on line 434
Array

Ulega: Uchanjaji wa mifugo bado unasuasua

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

SERIKALI imesema suala la uchanjaji wa mifugo bado lipo nchini hivyo imepanga kushirikiana na sekta binafsi kufanya kampeni ya chanjo nchi nzima ili kuokoa mifugo hiyo.

Hayo ameeezwa leo Septemba 6, 2023 jijini Dar es Salaam na Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulenga wakati akifungua mkutano wa pembeni wa Jukwaa la Mifumo ya Chakula Afrika (AGRF) unaoendelea nchini uliowakutanisha mawaziri wa uvuvi na mifugo na wadau katika sekta hiyo wenye lengo la kuelezea fursa zinazopatika nchini katika sekta ya hiyo.

Amesema Tanzania ina fursa nyingi za Uwekezaji kwenye Sekta ya uzalishaji wa chakula cha mifugo na kuwataka wawekezaji kutoka maeneo mbalimbali duniani kuja kuwekeza kwenye eneo hilo

“Hatua hiyo itasaidia kuipa Tanzania uwezo wa kusomeka katika ramani ya dunia kuwa inauwezo wa kupambana na magonjwa hasa yanayoonekana kuwa na uwezo wa kuambukiza hata binaadamu,” amesema Ulega.

Amesema kwa upande wa ufugaji wa kisasa asilimia 100 wanafanya chanjo huku kwa ufugaji wa asili ikiwa ni asilimia 20 pekee.

Akizungumzia kuhusu malisho, Ulega amefafanua kuwa Wizara ya Mifugo, Wizara ya Kilimo na Wizara ya Fedha zote kwa pamoja zimeonyesha utayari wa Serikali katika kuhakikisha suala la upatikanaji wa malisho ya uhakika ili ng’ombe wasiendelee kufa kwa ukame.

Ameongeza kuwa hata wazalishaji wa kuku wakati wa kiangazi wanapata wakati mgumu wa malisho kwa kuwa mahindi huwa yanapanda bei sana na hivyo gharama kuongezela gharama ya uzalishaji.

Amesema wamezungumza kwa pamoja na wadau ikiwa ni pamoja na kuwapati ardhi ili wafanyekazi ya uzalishaji.

Ameongeza kuwa wao kama wasaidizi wa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan wameonyesha utayari wa kuhakikisha wanatatua changamoto zinazoikabili sekta ya uzalishaji nchini hasa kwa kuyaleta pamoja makundi ya vijana na akinamama katika uzalishaji.

Naye Mwekezaji Sekta ya Mifugo, Mariam Sekuwe amesema akiwa mfugaji anayemiliki ng’ombe zaidi ya 100 na mmiliki wa kiwanda cha kusindika maziwa wanayo furaha kuona jukwaa la AGRF linakuwa fursa katika kupanua wigo wa uwezeshaji wa sekta ya mifugo nchini.

spot_img

Latest articles

Baraza la saba la Wafanyakazi Wizara ya Nishati lakutana Dodoma

📌 Dkt. Kazungu asema Wizara itaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya Kimkakati 📌 Baraza lapitisha rasimu...

Wizara ya Nishati yataja mafanikio utekelezaji majukumu 2024/25

📌 Uzalishaji umeme waongezeka kwa asilimia 59.9 📌 Misheni 300 kuongeza upatikanaji umeme...

Gavana Tutuba: Hali ya uchumi wa Tanzania inaendelea kuimarika

Na Tatu Mohamed GAVANA wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Emmanuel Tutuba amesema kuwa, hali...

Dkt. Biteko: Ufundi Stadi umepewa kipaumbele na serikali

📌 Asisitiza kuwa, Rais Samia anajenga vyuo kila wilaya nchini 📌 Apongeza utoaji wa mafunzo...

More like this

Baraza la saba la Wafanyakazi Wizara ya Nishati lakutana Dodoma

📌 Dkt. Kazungu asema Wizara itaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya Kimkakati 📌 Baraza lapitisha rasimu...

Wizara ya Nishati yataja mafanikio utekelezaji majukumu 2024/25

📌 Uzalishaji umeme waongezeka kwa asilimia 59.9 📌 Misheni 300 kuongeza upatikanaji umeme...

Gavana Tutuba: Hali ya uchumi wa Tanzania inaendelea kuimarika

Na Tatu Mohamed GAVANA wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Emmanuel Tutuba amesema kuwa, hali...