Warning: Array to string conversion in /home/themedia/domains/themediabrains.com/public_html/wp-includes/shortcodes.php on line 434
Array

Ulega: Uchanjaji wa mifugo bado unasuasua

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

SERIKALI imesema suala la uchanjaji wa mifugo bado lipo nchini hivyo imepanga kushirikiana na sekta binafsi kufanya kampeni ya chanjo nchi nzima ili kuokoa mifugo hiyo.

Hayo ameeezwa leo Septemba 6, 2023 jijini Dar es Salaam na Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulenga wakati akifungua mkutano wa pembeni wa Jukwaa la Mifumo ya Chakula Afrika (AGRF) unaoendelea nchini uliowakutanisha mawaziri wa uvuvi na mifugo na wadau katika sekta hiyo wenye lengo la kuelezea fursa zinazopatika nchini katika sekta ya hiyo.

Amesema Tanzania ina fursa nyingi za Uwekezaji kwenye Sekta ya uzalishaji wa chakula cha mifugo na kuwataka wawekezaji kutoka maeneo mbalimbali duniani kuja kuwekeza kwenye eneo hilo

“Hatua hiyo itasaidia kuipa Tanzania uwezo wa kusomeka katika ramani ya dunia kuwa inauwezo wa kupambana na magonjwa hasa yanayoonekana kuwa na uwezo wa kuambukiza hata binaadamu,” amesema Ulega.

Amesema kwa upande wa ufugaji wa kisasa asilimia 100 wanafanya chanjo huku kwa ufugaji wa asili ikiwa ni asilimia 20 pekee.

Akizungumzia kuhusu malisho, Ulega amefafanua kuwa Wizara ya Mifugo, Wizara ya Kilimo na Wizara ya Fedha zote kwa pamoja zimeonyesha utayari wa Serikali katika kuhakikisha suala la upatikanaji wa malisho ya uhakika ili ng’ombe wasiendelee kufa kwa ukame.

Ameongeza kuwa hata wazalishaji wa kuku wakati wa kiangazi wanapata wakati mgumu wa malisho kwa kuwa mahindi huwa yanapanda bei sana na hivyo gharama kuongezela gharama ya uzalishaji.

Amesema wamezungumza kwa pamoja na wadau ikiwa ni pamoja na kuwapati ardhi ili wafanyekazi ya uzalishaji.

Ameongeza kuwa wao kama wasaidizi wa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan wameonyesha utayari wa kuhakikisha wanatatua changamoto zinazoikabili sekta ya uzalishaji nchini hasa kwa kuyaleta pamoja makundi ya vijana na akinamama katika uzalishaji.

Naye Mwekezaji Sekta ya Mifugo, Mariam Sekuwe amesema akiwa mfugaji anayemiliki ng’ombe zaidi ya 100 na mmiliki wa kiwanda cha kusindika maziwa wanayo furaha kuona jukwaa la AGRF linakuwa fursa katika kupanua wigo wa uwezeshaji wa sekta ya mifugo nchini.

spot_img

Latest articles

Mwigulu rasmi Waziri Mkuu wa Tanzania

Na Mwandishi Wetu Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limemthibitisha Dk. Mwigulu Nchemba, kuwa...

Oktoba 29 siku ya giza, ifungue milango ya haki

OKTOBA 29, 2025 itabakia kuwa siku ya giza na machungu katika historia ya Jamhuri...

Fountain Gate yatoa kocha bora

Na Mwandishi Wetu Kocha wa timu ya Fountain Gate,  Mohamed Laizer amechaguliwa kuwa kocha bora...

Nyota JKT Queens aipigia hesabu Asec Mimosa

Na Winfrida Mtoi Mshambuliaji wa JKT Queens FC, Jamila Rajabu, amesema  amejipanga  kutengeneza  nafasi na...

More like this

Mwigulu rasmi Waziri Mkuu wa Tanzania

Na Mwandishi Wetu Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limemthibitisha Dk. Mwigulu Nchemba, kuwa...

Oktoba 29 siku ya giza, ifungue milango ya haki

OKTOBA 29, 2025 itabakia kuwa siku ya giza na machungu katika historia ya Jamhuri...

Fountain Gate yatoa kocha bora

Na Mwandishi Wetu Kocha wa timu ya Fountain Gate,  Mohamed Laizer amechaguliwa kuwa kocha bora...