Jeshi la polisi kuendelea kutumia TEHAMA katika kupambana na uhalifu nchini

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Jeshi la Polisi limesema litaendelea kutumia Tehama na mifumo katika kupambana na uhalifu wa kimtandao hapa Nchini,kutokana na Mabadiliko ya sayansi na Teknolojia na Ulimwengu wa sasa ambao wahalifu wamekuwa wakiutumia kutenda uhalifu.

Hayo ameyasema leo Agosti 17,2023 na Mkuu wa Chuo cha Taaluma ya Polisi Dar es Salaam (DPA) Kamishna msaidizi Mwandamizi wa Polisi, SACP Dk. Lazaro Mambosasa wakati akipokea Kompyuta kutoka kwa kampuni ya Sura Technologies Company Limited ya jijini Dar es Salaam ambapo amebainisha kuwa kompyuta hizo zitasaidia katika ufundishaji kwa askari walioko katika mafunzo.

Dk. Mambosasa amebainisha kuwa kompyuta hizo ni za kisasa ambazo zitawasaidia wakufunzi katika kufundisha wanafunzi waliopo katika chuo cha Taaluma ya Polisi Dar es Salaam (DPA) huku akitoa rai kwa wanafunzi kutumia vifaa hivyo vizuri ili viwanufanishe katika kupata mafunzo ya Tehama ambayo ndio dira ya Dunia kwa sasa.

Kwa upande wake, Edmund Mbao kutoka Sura Technologies Company Limited amesema kuwa wao kama wadau wa kupinga maswala ya kihalifu waliona ni vyema watoe vifaa hivyo vya Tehama kwa Jeshi la Polisi ambalo linahusika moja kwa moja na mapambano ya uhalifu hapa Nchini ambapo amebainisha kuwa wanaamini vifaa hivyo vinakwenda kutumika katika kufundisha askari ambao watapata mafunzo ya Tehama ili kukabiliana na uhalifu wa kimtandao hapa Nchini.

Naye Mkufunzi Mkuu wa chuo cha Taaluma ya Polisi Dar es Salaam, Kamishna msadizi wa Polisi ACP Andrea Legembo amesema kuwa kompyuta hizo zitakwenda kuongeza ufanisi wa ufundishaji wa Tehama kwa wanafunzi na wakufunzi wa chuo cha Taaluma ya Polisi Dar es Salaam (DPA).

spot_img

Latest articles

Mavazi ya kitamaduni kivutio kingine AFCON 2025

Na Winfrida Mtoi SHAMRASHAMRA kuelekea Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON-2025), zimezidi kupamba moto, hasa baada...

Livembe: Mchakato wa Uchaguzi ulikuwa wa haki na halali

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania (JWT), Hamis Livembe, amesema mchakato wa...

Sekta ya Viwanda na Biashara yazidi kutoa fursa kwa vijana

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Viwanda na Biashara, Judith Kapinga amesema sekta ya viwanda...

Polisi yachunguza tukio la kuchoma moto magari msibani

Na Mwandishi Wetu JESHI la Polisi Mkoa wa Morogoro limesema linachunguza tukio la kuchoma moto na...

More like this

Mavazi ya kitamaduni kivutio kingine AFCON 2025

Na Winfrida Mtoi SHAMRASHAMRA kuelekea Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON-2025), zimezidi kupamba moto, hasa baada...

Livembe: Mchakato wa Uchaguzi ulikuwa wa haki na halali

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania (JWT), Hamis Livembe, amesema mchakato wa...

Sekta ya Viwanda na Biashara yazidi kutoa fursa kwa vijana

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Viwanda na Biashara, Judith Kapinga amesema sekta ya viwanda...