Jeshi la polisi kuendelea kutumia TEHAMA katika kupambana na uhalifu nchini

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Jeshi la Polisi limesema litaendelea kutumia Tehama na mifumo katika kupambana na uhalifu wa kimtandao hapa Nchini,kutokana na Mabadiliko ya sayansi na Teknolojia na Ulimwengu wa sasa ambao wahalifu wamekuwa wakiutumia kutenda uhalifu.

Hayo ameyasema leo Agosti 17,2023 na Mkuu wa Chuo cha Taaluma ya Polisi Dar es Salaam (DPA) Kamishna msaidizi Mwandamizi wa Polisi, SACP Dk. Lazaro Mambosasa wakati akipokea Kompyuta kutoka kwa kampuni ya Sura Technologies Company Limited ya jijini Dar es Salaam ambapo amebainisha kuwa kompyuta hizo zitasaidia katika ufundishaji kwa askari walioko katika mafunzo.

Dk. Mambosasa amebainisha kuwa kompyuta hizo ni za kisasa ambazo zitawasaidia wakufunzi katika kufundisha wanafunzi waliopo katika chuo cha Taaluma ya Polisi Dar es Salaam (DPA) huku akitoa rai kwa wanafunzi kutumia vifaa hivyo vizuri ili viwanufanishe katika kupata mafunzo ya Tehama ambayo ndio dira ya Dunia kwa sasa.

Kwa upande wake, Edmund Mbao kutoka Sura Technologies Company Limited amesema kuwa wao kama wadau wa kupinga maswala ya kihalifu waliona ni vyema watoe vifaa hivyo vya Tehama kwa Jeshi la Polisi ambalo linahusika moja kwa moja na mapambano ya uhalifu hapa Nchini ambapo amebainisha kuwa wanaamini vifaa hivyo vinakwenda kutumika katika kufundisha askari ambao watapata mafunzo ya Tehama ili kukabiliana na uhalifu wa kimtandao hapa Nchini.

Naye Mkufunzi Mkuu wa chuo cha Taaluma ya Polisi Dar es Salaam, Kamishna msadizi wa Polisi ACP Andrea Legembo amesema kuwa kompyuta hizo zitakwenda kuongeza ufanisi wa ufundishaji wa Tehama kwa wanafunzi na wakufunzi wa chuo cha Taaluma ya Polisi Dar es Salaam (DPA).

spot_img

Latest articles

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

More like this

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...