UTT AMIS kutoa elimu zaidi ya uwekezaji

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Ukosefu wa elimu ya mifumo ya imatajwa kuwa miongoni mwa changamoto kubwa inayowakabili watu wanaowekeza kwenye mifuko ya uwekezaji nchini.

Hayo yamebainishwa Dar es Salaam Jumatatu Julai 31, 2023 na Mkurugenzi Mtendaji wa UTT Amis, Simon Migangala wakati wa mkutano na Wahariri na Waandishi wa Habari kuhusu mafanikio ya kampuni hiyo.

Amesema pamoja na kwamba kumekuwa na mwitikio mkubwa kwa Watanzania kujitokeza kuwekeza na mifuko iliyo chini ya kampuni hiyo, lakini bado elimu zaidi inahitajika.

“Tunashukuru kwamba mifuko yetu yote imekuwa ikienda vizuri, lakini UTT Amis tunakabiriwa na changamoto mbalimbali ikiwemo watu wengi kukosa uelewa na elimu ya masoko ya fedha.

“Pia wengi bado hawana kipato kikubwa cha kuwekeza, mtu anaona kwamba kutumia fedha badala ya kuiwekeza kwa ajili ya malengo ya baadaye, tumezingatia shida zetu kuliko kuwekeza,” amesema Migangala.

Amesema katika kukabiliana na changamoto hiyo watahakikisha kwamba wanatoa elimu zaidi kwa wananchi ikiwamo kutumia vyombo vya habari ili kujenga uelewa kuhusu mifumo hiyo ya uwekezaji.

Katika hatua nyingine amesema UTT Amis imeboreshwa kwa uwekezaji wenye malengo ya muda mrefu na muda mfupi ili kuhakikisha kila Mtazania anawekeza kwa maslahi yake na taifa kwa ujumla.

“Maisha yetu tunategemea fedha ikiwa tofauti na miaka ya zamani kwa wengi tulikuwa tunarithishwa aridhi lakini sasa hivi urithi wetu unategemea kwenye uwekezaji wa fedha hivyo niwahimize kuwekeza UTT AIMS kwani kila Mtanzania atajivunia,” amesema Mgangala.

Akizungumzia mafanikio ya miaka minne mfululizo waliopata kutokana na uwekezaji mdogo na mkubwa wameweza kuchangia katika Pato la Taifa.

“Mafanikio haya ni kwa mwaka juzi ukuaji wa taasisi kutoka Sh bilioni 600 hadi Sh bilioni 996 sawa na asilimia 50 kwa mwaka 2022 kutoka Sh bilioni 996 hadi Sh Trilioni 1. 5 sawa na asilimia 54 ukuaji huu umeenda vizuri ikilinganishwa na kipindi cha nyuma,” amesema Mgangala.

Amesema kwa mwaka wa fedha ulioishia Juni, mwaka huu ukuaji umeongezeka kwa asilimia 12 kwa miaka sita huku wakitoa gawio kwa serikalini.

Aidha, amewataka Watanzania kuendelea kuwekeza kwasababu taasisi hiyo iko imara na kwamba kufanya hivyo ni fursa kwa maisha ya baadaye.

Naye, Mkurugenzi wa Masoko UTT Amis, Daud Mbaga amesema lengo lolote lazima liwe na muda katika kuwekeza kwenye fedha na mtaji.

Amesema kwa kiasi kikubwa wameweza kufanikiwa kutoa elimu vyuoni hadi shule ya msingi hivyo wawekezaji wengi ni wanafunzi, walimu na wengine.

“Watu waliofikiwa na elimu ya UTT Amis hatupimi kwa asilimia hivyo Tanzania inazaidi ya vijiji 3,000, hivyo tunakutana na watu mbalimbali kuhakikisha kwamba inamfikia kila mtu,” amesema Mbaga.

Amesema wanamkakati wa kuongeza somo la uwekezaji liingie shule ya msingi na na ngazi nyingine za elimu ili wanafunzi wajue umuhimu wa kuwekeza na faida na shughuli za UTT Amis.

Akifafanua zaidi amesema UTT Amis wamefanikiwa kujitanua zaidi katika kuhakikisha kuwa wanafika kwenye maeneo mengi wanakopatikana wawekezaji hususan Mikoa mbalimbali ya Tanzania.

“Tuna ofisi Arusha, Dodoma na Dar es Salaam na kiwngine pia tuna mawakala  nchi nzima kupitia matawi ya benki ya CRDB ambapo wawekezaji wetu wanapata huduma.

“Hapo awali ilimbidi mwekezaji wetu aende benki moja kwa moja ili kununua vipande, lakini kwasasa Mwekezaji anaweza kununua vipande kupitia njia zote za malipo za benki ya CRDB yaani Simbanking, CRDB App na Fahari Huduma.

“Pia kwa kutumia simu ya mkononi huduma za  Tigopesa, Airtel Money, M-Pesa, T-pesa na Halopesa inawezekana kununua vipande. Hali kadhalika kwa kutumia program tumizi (App) za benki ya Amana na  Standard Charter mwekezaji anaweza kununua vipande moja kwa moja. Hivyo ni bayana kuwa teknolojia imekuwa nyenzo muhimu katika kusaidia kuwafikia na kuwahudumia wawekezaji wetu kwa urahisi,” amesema.

spot_img

Latest articles

Tuna deni la kusimamia miradi na kusikiloza kero za wananchi ili kuleta Maendeleo ya kweli: Salome

Na Mwandishi Wetu NAIBU Waziri wa Nishati, Salome Makamba, amesema viongozi wana deni kubwa...

2025 mwaka wa mageuzi na matokeo katika mashirika ya umma

Na Mwandishi Wetu MWAKA 2025 ulikuwa wa mafanikio makubwa kwa Ofisi ya Msajili wa...

Wakatoliki feki wamechafua hali ya hewa, aibu hii anabeba nani?

TAHARUKI kubwa imeibuka nchini. Unaweza kuiona ukichungulia kwenye mitandao ya kijamii. Imesababishwa na akili...

Mukwala atua Zanzibar, Simba ikiivaa Azam kesho Mapinduzi Cup

Na Winfrida Mtoi WAKATI Simba kitarajia kukabiliana na Azam FC kesho katika mchezo wa nusu...

More like this

Tuna deni la kusimamia miradi na kusikiloza kero za wananchi ili kuleta Maendeleo ya kweli: Salome

Na Mwandishi Wetu NAIBU Waziri wa Nishati, Salome Makamba, amesema viongozi wana deni kubwa...

2025 mwaka wa mageuzi na matokeo katika mashirika ya umma

Na Mwandishi Wetu MWAKA 2025 ulikuwa wa mafanikio makubwa kwa Ofisi ya Msajili wa...

Wakatoliki feki wamechafua hali ya hewa, aibu hii anabeba nani?

TAHARUKI kubwa imeibuka nchini. Unaweza kuiona ukichungulia kwenye mitandao ya kijamii. Imesababishwa na akili...