PURA yaja na suluhu ya ukosefu wa vyeti vya usalama baharini

Na Mwandishi Wetu, Zanzibar

Mamlaka ya Udhibiti mkondo wa juu wa petroli (PURA) imebainisha mikakati inayoendelea kutekelezwa ikiwemo kutatua changamoto ya ukosefu wa vyeti vya masuala ya usalama baharini jambo ambalo limekuwa likidumaza ushiriki wa Watanzania katika miradi ya mafuta na gesi asilia.

Mkuu wa Kitengo cha Ushirikishwaji wa Wazawa na Uhusishwaji wa Wadau PURA,Charles Nyangi.

Hayo yamebainishwa Julai 26 Visiwani Zanzibar wakati aikichangia mjadala kuhusu changamoto zinazozuia watanzania wenye ujuzi stahiki kushiriki kikamilifu Katika miradi ya mafuta na gesi asilia kwenye Kongamano la Nishati na Madini na Mkuu wa Kitengo cha Ushirikishwaji wa Wazawa na Uhusishwaji wa Wadau wa Mamlaka hiyo, Charles Nyangi amesema watanzania kushiriki katika miradi ya utafutaji na uzalishaji wa gesi asilia nchini hususan miradi inayotekelezwa maeneo ya baharini.

Amesema miradi inayotekelezwa nchini na mikakati ambayo PURA inatekeleza kutatua changamoto hizo.

“Akiongelea mkakati wa kutatua moja ya changamoto aliyoitaja kama ukosefu wa vyeti vya masuala ya usalama ili kuweza kufanya kazi maeneo ya baharini, alieleza kuwa PURA iko mbioni kusaini Makubaliano ya Awali na Chuo cha Bahari Dar es Salaam(DMI) kwa lengo la kushirikiana kuanzisha kituo chenye ithibati kinachotambulika duniani kitakachotoa mafunzo hayo nchini,” amesema Nyangi.

Amesema kwa sasa hakuna kituo chenye ithibati nchini Tanzania kinachotoa kozi za masuala ya usalama na tahadhari kama vile Basic Offshore Safety Induction and Emergency Training (BOSIET) yanayowezesha mtu kupata kibali cha kufanya kazi katika miradi ya mafuta na gesi inayotekelezwa baharini.

Nyangi amesema Chagamoto hiyo imepeleka watanzania wenye ujuzi na uwezo wa kufanya kazi katika miradi hiyo kulazimika kwenda nje ya nchi kwa gharama kubwa kusomea kozi hizo.

Amesema hiyo ni changamoto kwa kuwa watanzania wachache ndio wanaoweza kumudu gharama za kwenda nje ya nchi kusoma kozi husiki.

Aidha amesema kuanzishwa kwa kituo hicho nchini, kutawezesha watanzania wengi zaidi kupata cheti cha usalama na umahiri baharini hivyo kusaidia ongezeko la watanzania wanaoshiriki katika miradi ya mafuta na gesi asilia hususan miradi ya mkondo wa juu wa petroli inayotekelezwa nchini.

spot_img

Latest articles

Aucho asimamishwa Singida Bs kwa utovu wa nidhamu

Na Mwandishi Wetu KIUNGO Khalid Aucho amesimamishwa kwa miezi mitatu na klabu yake ya Singida...

Ngome ya Wanawake ACT Wazalendo yatangaza Machi kuwa Mwezi wa Maombolezo

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Ngome ya Wanawake ya ACT Wazalendo, Janeth Rithe, ametangaza...

Haikubaliki, hali hii ya D’Salaam inachefua

KATIKA siku za hivi karibuni kumekuwa na matamko ya operesheni mbalimbali za kurejesha uzingatiaji...

Mwanasheria Mkuu asisitiza mageuzi ya Sheria za Anga

Na Mwandishi Wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesisitiza juu ya umuhimu wa...

More like this

Aucho asimamishwa Singida Bs kwa utovu wa nidhamu

Na Mwandishi Wetu KIUNGO Khalid Aucho amesimamishwa kwa miezi mitatu na klabu yake ya Singida...

Ngome ya Wanawake ACT Wazalendo yatangaza Machi kuwa Mwezi wa Maombolezo

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Ngome ya Wanawake ya ACT Wazalendo, Janeth Rithe, ametangaza...

Haikubaliki, hali hii ya D’Salaam inachefua

KATIKA siku za hivi karibuni kumekuwa na matamko ya operesheni mbalimbali za kurejesha uzingatiaji...