PURA yaja na suluhu ya ukosefu wa vyeti vya usalama baharini

Na Mwandishi Wetu, Zanzibar

Mamlaka ya Udhibiti mkondo wa juu wa petroli (PURA) imebainisha mikakati inayoendelea kutekelezwa ikiwemo kutatua changamoto ya ukosefu wa vyeti vya masuala ya usalama baharini jambo ambalo limekuwa likidumaza ushiriki wa Watanzania katika miradi ya mafuta na gesi asilia.

Mkuu wa Kitengo cha Ushirikishwaji wa Wazawa na Uhusishwaji wa Wadau PURA,Charles Nyangi.

Hayo yamebainishwa Julai 26 Visiwani Zanzibar wakati aikichangia mjadala kuhusu changamoto zinazozuia watanzania wenye ujuzi stahiki kushiriki kikamilifu Katika miradi ya mafuta na gesi asilia kwenye Kongamano la Nishati na Madini na Mkuu wa Kitengo cha Ushirikishwaji wa Wazawa na Uhusishwaji wa Wadau wa Mamlaka hiyo, Charles Nyangi amesema watanzania kushiriki katika miradi ya utafutaji na uzalishaji wa gesi asilia nchini hususan miradi inayotekelezwa maeneo ya baharini.

Amesema miradi inayotekelezwa nchini na mikakati ambayo PURA inatekeleza kutatua changamoto hizo.

“Akiongelea mkakati wa kutatua moja ya changamoto aliyoitaja kama ukosefu wa vyeti vya masuala ya usalama ili kuweza kufanya kazi maeneo ya baharini, alieleza kuwa PURA iko mbioni kusaini Makubaliano ya Awali na Chuo cha Bahari Dar es Salaam(DMI) kwa lengo la kushirikiana kuanzisha kituo chenye ithibati kinachotambulika duniani kitakachotoa mafunzo hayo nchini,” amesema Nyangi.

Amesema kwa sasa hakuna kituo chenye ithibati nchini Tanzania kinachotoa kozi za masuala ya usalama na tahadhari kama vile Basic Offshore Safety Induction and Emergency Training (BOSIET) yanayowezesha mtu kupata kibali cha kufanya kazi katika miradi ya mafuta na gesi inayotekelezwa baharini.

Nyangi amesema Chagamoto hiyo imepeleka watanzania wenye ujuzi na uwezo wa kufanya kazi katika miradi hiyo kulazimika kwenda nje ya nchi kwa gharama kubwa kusomea kozi hizo.

Amesema hiyo ni changamoto kwa kuwa watanzania wachache ndio wanaoweza kumudu gharama za kwenda nje ya nchi kusoma kozi husiki.

Aidha amesema kuanzishwa kwa kituo hicho nchini, kutawezesha watanzania wengi zaidi kupata cheti cha usalama na umahiri baharini hivyo kusaidia ongezeko la watanzania wanaoshiriki katika miradi ya mafuta na gesi asilia hususan miradi ya mkondo wa juu wa petroli inayotekelezwa nchini.

spot_img

Latest articles

Mchezo wa kuogelea wazidi kupaa nchini, TSA  yafichua siri

Na Winfrida  Mtoi MCHEZO wa kuogelea umezidi kushika kasi nchini  kutokana na kuongezeka idadi ya...

Dkt Nchimbi atembelea banda la Tanesco

Na Mwandishi Wetu MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi...

Waogeleaji chipukizi 400 kutikisa Dar kesho

Na Mwandishi Wetu Zaidi ya waogeleaji 400 wenye umri wa miaka 6 hadi 12 wanatarajiwa...

Wabunge walifuata mkumbo kwenda Morocco kuishangilia Serengeti Boys lawakuta jambo

Na Mwandishi Wetu SPIKA wa Mbunge la Tanzania, Mussa Azzan Zungu ametoa siku nne za...

More like this

Mchezo wa kuogelea wazidi kupaa nchini, TSA  yafichua siri

Na Winfrida  Mtoi MCHEZO wa kuogelea umezidi kushika kasi nchini  kutokana na kuongezeka idadi ya...

Dkt Nchimbi atembelea banda la Tanesco

Na Mwandishi Wetu MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi...

Waogeleaji chipukizi 400 kutikisa Dar kesho

Na Mwandishi Wetu Zaidi ya waogeleaji 400 wenye umri wa miaka 6 hadi 12 wanatarajiwa...