Sheikh Jalala ataka mabadiliko mwaka mpya wa Kiislamu

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Waumini wa dini ya Kiislamu wametakiwa kuendelea kuenzi umoja na mshikamano wa kitaifa katika mwaka mpya wa Kiislamu 1445.

Mwaka Mpya wa Kiislamu ni siku muhimu katika kalenda ya Kiislamu duniani kote na huadhimishwa kila mwaka.

Wito huo umetolewa Dar es Salaam Julai 18,2023 na Sheikh Mkuu wa Jumuiya ya Shia Ithnashaari, Hemed Jalala, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mwaka mpya wa Kiislamu.

Amewataka waislamu wajitathmini mwaka uliopita wapi wamefanikiwa, walikokwama na namna watakavyoweza kusonga mbele.

Sheikh Jalala pia amesisitiza mwaka mpya wa kiislamu uwe wa kuenzi umoja wa Watanzania wote bila kujali tofauti zao na dini zao.

“Mwaka 1445 uwe ni mwaka wa umoja, mshikamano, tuungane na kuwa kitu kimoja na kuhimiza umoja. Waislamu umefika muda wa kuacha tofauti zetu na kukaa meza moja.

“Umoja wa Watanzania ni muhimu mno, umoja wa kitaifa, kupenda Tanzania yetu ni moja kati ya misingi muhimu. Tuhubiri umoja kati ya sisi waislamu na ndugu zetu wakristo, tuhakikishe dini hizi zinashikamana, zinakaa vizuri na zinapendana,” amesema Sheikh Jalala.

Amewahimiza viongozi wa dini kuhubiri zaidi kuhusu mmomonyoko wa maadili ili vijana wawe na maadili mema yanayompendeza Mungu.

Waislamu wanasherehekea mwaka mpya wakimkumbuka pia Imamu Hussein ambaye aliuawa akipigania kurudisha maadili, mshikamano, umoja na amani katika jamii.

spot_img

Latest articles

Mhudumu wa mochwari mbaroni kwa tuhuma za kukutwa na viungo vya binadamu

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi mkoani Kagera linawashikilia watu wawili akiwamo mhudumu wa mochwari...

Katibu wa fedha UVCCM Dar arudisha fomu ya ridhaa ya ubunge Kawe

Katibu wa Uchumi, Mipango na Fedha UVCCM Mkoa wa Dar es Salaam, Hassan Ali...

Majaliwa  atangaza hagombei tena ubunge Ruangwa

Na Mwandishi Wetu Waziri mkuu na Mbunge wa Jimbo la Ruangwa, Kassim Majaliwa leo Julai...

Vijana, Dira na CCM. Chama pekee chenye Imani na vijanaTangu kuasisiwa

Na Mwandishi Wetu TANGU kuasisiwa kwake tarehe 5 Februari 1977 kwa muungano wa TANU...

More like this

Mhudumu wa mochwari mbaroni kwa tuhuma za kukutwa na viungo vya binadamu

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi mkoani Kagera linawashikilia watu wawili akiwamo mhudumu wa mochwari...

Katibu wa fedha UVCCM Dar arudisha fomu ya ridhaa ya ubunge Kawe

Katibu wa Uchumi, Mipango na Fedha UVCCM Mkoa wa Dar es Salaam, Hassan Ali...

Majaliwa  atangaza hagombei tena ubunge Ruangwa

Na Mwandishi Wetu Waziri mkuu na Mbunge wa Jimbo la Ruangwa, Kassim Majaliwa leo Julai...