Warning: Array to string conversion in /home/themedia/domains/themediabrains.com/public_html/wp-includes/shortcodes.php on line 434
Array

Rais Samia: Majirani watatumia fursa ya sisi kulumbana kunufaisha bandari zao

*Prof. Mbarawa awekezaji ukikamilika utachangia asilimia 67 ya bajeti

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, ameweka msimamo wa uwekezaji wa Bandari kupitia Kampuni ya DP World, akisema malumbano hayawezi kupewa nafasi kwenye mkakati wa kiuchumi.

Rais wa Samia ameyasema hayo leo Ijumaa Julai 14, 2023 wakati wa kuwaapisha Viongozi wateule hafla iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam, ikiwa ni mwendelezo wa Serikali kutoa ufafanuzi kuhusu baadhi ya watu wanaotumia muda mwingi kurumbana, hali inayochelewesha uwekezaji huo na kutoa mwanya kwa majirani zao kuweka nia ya kupita njia wanayopitia.

“Ndugu zangu wakati sisi tunalumbana kuhusu huu uwekezaji, wenzetu tumeona nao wakionesha njia ya kutafuta mtu wa kuwekeza kwenye bandari yao,” amesema Rais Samia.

Mara baada ya Serikali kutangaza mpango wa kuwekeza kwenye bandari ya Dar es Salaam, baadhi ya wanasiasa na wanaharakati wamekuwa wakipinga, hali iliyomuibua Rais Samia kutoa ufafanuzi.

Mapema leo Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa akizungumza kakao na Wahariri na waandishi wa Vyombo vya habari nchini amesema kuwa karibu dunia nzima kampuni binafsi ndizo zinaendesha bandari.

“Ukiangalia kuna kampuni 10 dunia ikiwamo DP World ambazo ndizo zinaendesha bandari mbalimbali, hivyo niwasihi Watanzania kwamba tuko katika njia sahihi na hii itaenda kubadilisha kabisa uchumi wa Taifa letu.

“Tunahitaji kuwatea maendeleo wananchi wetu, kama tutaweza kupata mwekezaji na kusimamia vizuri bandari yetu basi asilimia 67 ya bajeti yetu yatatoka bandarini,”  amesema Profesa Mbarawa.

spot_img

Latest articles

Watahiniwa 595,816 kuanza Mtihani wa Kidato cha Nne kesho

Na Tatu Mohamed JUMLA ya watahiniwa 595,816 wamesajiliwa kufanya Mtihani wa Kidato cha Nne 2025...

Tume kuundwa kuchunguza vurugu zilizotokea Oktoba 29, mwaka huu

Na Mwandishi Wetu  RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametangaza...

Mkakati wa Mawasiliano wa Nishati Safi ya kupikia: Dira ya Mafanikio ya Taifa

Na Mwandishi Wetu IMEELEZWA kuwa Mkakati wa Mawasiliano wa Nishati Safi ya Kupikia ni...

JKT Queens na matumaini nusu  fainali CAFWCL mbele ya TP Mazembe

Na Mwandishi Wetu Baada ya timu ya JKT Queens kutoa sare mbili mfululizo Ligi ya...

More like this

Watahiniwa 595,816 kuanza Mtihani wa Kidato cha Nne kesho

Na Tatu Mohamed JUMLA ya watahiniwa 595,816 wamesajiliwa kufanya Mtihani wa Kidato cha Nne 2025...

Tume kuundwa kuchunguza vurugu zilizotokea Oktoba 29, mwaka huu

Na Mwandishi Wetu  RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametangaza...

Mkakati wa Mawasiliano wa Nishati Safi ya kupikia: Dira ya Mafanikio ya Taifa

Na Mwandishi Wetu IMEELEZWA kuwa Mkakati wa Mawasiliano wa Nishati Safi ya Kupikia ni...