Warning: Array to string conversion in /home/themedia/domains/themediabrains.com/public_html/wp-includes/shortcodes.php on line 434
Array

Rais Samia: Majirani watatumia fursa ya sisi kulumbana kunufaisha bandari zao

*Prof. Mbarawa awekezaji ukikamilika utachangia asilimia 67 ya bajeti

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, ameweka msimamo wa uwekezaji wa Bandari kupitia Kampuni ya DP World, akisema malumbano hayawezi kupewa nafasi kwenye mkakati wa kiuchumi.

Rais wa Samia ameyasema hayo leo Ijumaa Julai 14, 2023 wakati wa kuwaapisha Viongozi wateule hafla iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam, ikiwa ni mwendelezo wa Serikali kutoa ufafanuzi kuhusu baadhi ya watu wanaotumia muda mwingi kurumbana, hali inayochelewesha uwekezaji huo na kutoa mwanya kwa majirani zao kuweka nia ya kupita njia wanayopitia.

“Ndugu zangu wakati sisi tunalumbana kuhusu huu uwekezaji, wenzetu tumeona nao wakionesha njia ya kutafuta mtu wa kuwekeza kwenye bandari yao,” amesema Rais Samia.

Mara baada ya Serikali kutangaza mpango wa kuwekeza kwenye bandari ya Dar es Salaam, baadhi ya wanasiasa na wanaharakati wamekuwa wakipinga, hali iliyomuibua Rais Samia kutoa ufafanuzi.

Mapema leo Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa akizungumza kakao na Wahariri na waandishi wa Vyombo vya habari nchini amesema kuwa karibu dunia nzima kampuni binafsi ndizo zinaendesha bandari.

“Ukiangalia kuna kampuni 10 dunia ikiwamo DP World ambazo ndizo zinaendesha bandari mbalimbali, hivyo niwasihi Watanzania kwamba tuko katika njia sahihi na hii itaenda kubadilisha kabisa uchumi wa Taifa letu.

“Tunahitaji kuwatea maendeleo wananchi wetu, kama tutaweza kupata mwekezaji na kusimamia vizuri bandari yetu basi asilimia 67 ya bajeti yetu yatatoka bandarini,”  amesema Profesa Mbarawa.

spot_img

Latest articles

Msajili wa Hazina aonya taasisi za umma zenye utendaji duni Dar es Salaam.

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imeonya taasisi za umma zinazofanya vibaya kujitathmini na kuchukua hatua za...

KAMATI YA BUNGE YA NISHATI NA MADINI YARIDHISHWA NA MAENDELEO YA UZALISHAJI UMEME KITUO CHA JULIUS NYERERE

📌Yasema Kituo kinachangia asilimia 45 ya umeme katika Gridi ya Taifa 📌Yasisitiza ukamilishaji wa miradi...

MD TWANGE AFAFANUA CHANZO CHA HITILAFU ILIYOTOKEA KWENYE GRIDI YA UMEME YA TAIFA

📌 Aomba radhi kwa wateja wananchi na kuwahakikishia upatikanaji endelevu wa huduma ya umeme 📌...

Hatuna pa kujificha, tuwajibike tu yaishe

TAIFA la Tanzania ni nchi huru iliyojitawala kwa takribani miaka 65 sasa, tangu bendera...

More like this

Msajili wa Hazina aonya taasisi za umma zenye utendaji duni Dar es Salaam.

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imeonya taasisi za umma zinazofanya vibaya kujitathmini na kuchukua hatua za...

KAMATI YA BUNGE YA NISHATI NA MADINI YARIDHISHWA NA MAENDELEO YA UZALISHAJI UMEME KITUO CHA JULIUS NYERERE

📌Yasema Kituo kinachangia asilimia 45 ya umeme katika Gridi ya Taifa 📌Yasisitiza ukamilishaji wa miradi...

MD TWANGE AFAFANUA CHANZO CHA HITILAFU ILIYOTOKEA KWENYE GRIDI YA UMEME YA TAIFA

📌 Aomba radhi kwa wateja wananchi na kuwahakikishia upatikanaji endelevu wa huduma ya umeme 📌...