Mhitimu wa VETA abuni mashine za kuongeza thamani ya mazao, ajiajiri kupitia kampuni yake

Na Mwandishi Wetu

MHITIMU wa mafunzo ya ufundi stadi kupitia VETA, Ernest Maranya, amebuni na kutengeneza mashine za kuongeza thamani ya mazao mbalimbali ya kilimo, hatua iliyomwezesha kujiajiri kwa kuanzisha kampuni inayotengeneza teknolojia za usindikaji wa mazao.

Maranya amesema kampuni yake yenye makao makuu jijini Dar es Salaam inatengeneza mashine za kusindika mazao mbalimbali, ikiwemo karanga, kahawa na karafuu, kwa lengo la kuwasaidia wakulima na wajasiriamali kuongeza thamani ya bidhaa zao kabla ya kuzipeleka sokoni.

Amesema mashine hizo huchakata mazao kwa ufanisi, jambo linaloboresha ubora wa bidhaa na kuongeza thamani yake sokoni, hivyo kuwawezesha wakulima na wafanyabiashara wadogo kupata faida zaidi.

Kwa mujibu wake, tayari ametoa huduma kwa wajasiriamali kutoka mikoa mbalimbali, ikiwemo Dar es Salaam, Arusha na Mbeya, ambapo baadhi yao wamefanikiwa kuanzisha au kupanua shughuli zao za uzalishaji kwa kutumia mashine hizo.

Maranya amesema ujuzi alioupata kupitia mafunzo ya VETA ndio uliomuwezesha kubuni mashine hizo na kuanzisha biashara yake, badala ya kusubiri ajira rasmi.

Amewahimiza vijana kujiunga na mafunzo ya ufundi stadi, akisema huwapa ujuzi wa vitendo unaowawezesha kujiajiri, kubuni teknolojia na kuanzisha biashara zinazotoa suluhisho kwa jamii.

Aidha, amesema mafanikio aliyoyapata yanaonesha kuwa ujuzi unaotolewa na VETA unaweza kuwa msingi wa kujikwamua kiuchumi, huku akiwataka vijana kuitumia fursa hiyo kwa bidii, ubunifu na kujituma.

spot_img

Latest articles

MHE.SALOME: WANANCHI WANAOPITIWA NA MIUNDOMBINU YA UMEME WAUNGANISHIWE HUDUMA KWA SH. 27,000

Na Mwandishi Wetu, Mara Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, amesema Serikali ya Awamu...

TTCL Yakabidhi Magari 6 ya Sh. Milioni 903 Kuimarisha Ufanisi wa Huduma

Na Mwandishi Wetu SHIRIKA la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limeendelea kutekeleza mkakati wake wa kuboresha...

Ofisi ya Usuluhishi wa Kodi Yaahidi Kuimarisha Mazingira ya Biashara na Uwekezaji

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Usuluhishi wa Malalamiko na Taarifa za Kodi imesema, inaendelea...

Mkondo wa amali waanza kuzaa matunda, wanafunzi waonesha ubunifu Sabasaba

Na Tatu Mohamed WANAFUNZI wanaosoma mkondo wa amali wameanza kuonesha matokeo ya ujuzi wa...

More like this

MHE.SALOME: WANANCHI WANAOPITIWA NA MIUNDOMBINU YA UMEME WAUNGANISHIWE HUDUMA KWA SH. 27,000

Na Mwandishi Wetu, Mara Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, amesema Serikali ya Awamu...

TTCL Yakabidhi Magari 6 ya Sh. Milioni 903 Kuimarisha Ufanisi wa Huduma

Na Mwandishi Wetu SHIRIKA la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limeendelea kutekeleza mkakati wake wa kuboresha...

Ofisi ya Usuluhishi wa Kodi Yaahidi Kuimarisha Mazingira ya Biashara na Uwekezaji

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Usuluhishi wa Malalamiko na Taarifa za Kodi imesema, inaendelea...