Yanga yakomaa kileleni, Simba yavizia ikitafuna  miwa Morogoro

Na Mwandishi Wetu

WANANCHI Yanga wamejiweka kwenye nafasi nzuri ya kutetea ubingwa wa Ligi Kuu Soka Tanzania Bara kwa mara ya tano mfululizo baada ya   ushindi wa 3-0 dhidi ya Azam FC katika dimba la New Amaan Complex, Zanzibar.

Mabao ya Yanga yamefungwa na Ibrahim Bacca dk 41, Laurindo Depu dk 73, Pacome  Zouzoua dk 81. Wanajangwani hao wamefikisha alama 69 katika michezo 28 waliyocheza na kuendelea  kusalia kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo.

Katika mchezo mwingine, Mnyama Simba ameibuka na ushindi wa 3-0 dhidi ya Mtibwa Sugar katika uwanja wa  Jamhuri, Morogoro huku akiendelea kusalia nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi   akiwa na alama 67 baada ya mechi 28.

Wafungaji wa Simba ni Rushine de Reuck dk 9’p, Selemani  Mwalimu dk 77’, Anicent Oura dk 90.

Mechi zilizobaki kwa vigogo hao wa Kariakoo, Yanga itacheza na TRA United nyumbani, kisha JKT Tanzania. Simba itakutana na Singida Bs na KMC, itakuwa nyumbani mechi zote.

Matokeo mengine ya mechi za raundi ya 28

 FT: Singida BS 3-1 TZ Prisons (Mossi 2’, 61’, Kennedy 23’ / Sengati 49’)
FT: TRA United 1-1 Coastal Union (Kombo 54’p / Maabad 68’p)
FT: Dodoma Jiji 0-0 JKT Tanzania
FT: Pamba Jiji 0-2 Mbeya City (Ambokile 18’, 76’)
FT: Fountain Gate 0-1 Mashujaa (Hussein Mihambo 86’)
FT: KMC 2-3 Namungo (Mwijage 36’, Mohamed 70’ / Ngoy 18’, 24’, 52’)

spot_img

Latest articles

WIZARA YA NISHATI YAENDELEA KUTUMIA NISHATI SAFI EXPO KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

Na Mwandishi Wetu WIZARA ya Nishati inaendelea kutoa elimu ya nishati safi ya kupikia...

Wiki ya Utumishi wa Umma yasogeza huduma za Taasisi za Umma karibu na wananchi

Na Mwandishi Wetu Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma ya mwaka 2026 yameonesha...

MADIWANI WA MPANDA NA NSIMBO WAIPONGEZA SERIKALI KWA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA KITUO CHA KUFUA UMEME CHA JULIUS NYERERE

Na Mwandishi wetu Rufiji - Pwani MADIWANI wa Halmashauri za Wilaya za Mpanda na Nsimbo mkoani...

WANANCHI MSIHOFU KUTUMIA NISHATI YA UMEME KATIKA VYOMBO VYA USAFIRI -MD TWANGE

📌Asema TANESCO inajenga vituo vya kuchajia vyombo hivyo nchi nzima 📌Aeleza mpango wa kusambaza majiko...

More like this

WIZARA YA NISHATI YAENDELEA KUTUMIA NISHATI SAFI EXPO KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

Na Mwandishi Wetu WIZARA ya Nishati inaendelea kutoa elimu ya nishati safi ya kupikia...

Wiki ya Utumishi wa Umma yasogeza huduma za Taasisi za Umma karibu na wananchi

Na Mwandishi Wetu Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma ya mwaka 2026 yameonesha...

MADIWANI WA MPANDA NA NSIMBO WAIPONGEZA SERIKALI KWA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA KITUO CHA KUFUA UMEME CHA JULIUS NYERERE

Na Mwandishi wetu Rufiji - Pwani MADIWANI wa Halmashauri za Wilaya za Mpanda na Nsimbo mkoani...