Na Mwandishi Wetu
MAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masijala Ndogo ya Dar es Salaam, imepanga kusilikiza shauri la Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu linalohusu maombi ya kuunganishwa katika kesi inayohusu mgawanyo wa mali za chama hicho.
Shauri hilo limetajwa leo Mei 25, 2026, mbele ya Jaji David Ngunyale, ambapo Mahakama imeutaka upande wa wajibu maombi kuwasilisha viapo vyao kinzani ndani ya siku saba.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kuahirishwa kwa shauri hilo, Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Dk. Rugemeleza Nshala, amesema hatima ya maombi ya Mwenyekiti huyo itategemea uamuzi unaotarajiwa kutolewa Mei 28, 2026 katika kesi ya msingi iliyorejeshwa Mahakama Kuu kutoka Mahakama ya Rufani.
Ameeleza kuwa, iwapo Mahakama itaamua kesi hiyo inaendelea kuwa na nguvu kisheria, basi maombi ya mwenyekiti yataendelea kusikilizwa, lakini kama kesi ya msingi itafutwa, hata maombi hayo yataathirika.


