TTB yamkaribisha bingwa wa Masumbwi duniani Terence kwa ziara ya utalii

Na Mwandishi Wetu

MKURUGENZI wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Ephraim Mafuru, amemkaribisha nchini kwa mara ya kwanza bingwa wa masumbwi duniani, Terence Crawford, ambaye katika historia yake hajawahi kupoteza pambano lolote.

Ziara hiyo ya wiki moja nchini imeandaliwa kwa ushirikiano kati ya Wizara ya Maliasili na Utalii pamoja na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuendeleza utalii wa michezo nchini.

Akizungumza Mei 24,2026, kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam wakati wa mapokezi ya mwanamasumbwi huyo, Mafuru amesema Serikali imeamua kutumia watu mashuhuri wenye ushawishi mkubwa duniani kuitangaza Tanzania kimataifa kupitia sekta ya utalii na michezo.

Amesema lengo la kampeni hiyo ni kukuza utalii wa michezo sambamba na kupata idadi kubwa ya watalii wanaoingia nchini na kuongeza muda wa kukaa kwao.

Mafuru ameeleza kuwa mbali na utalii wa wanyamapori, fukwe, utamaduni na mikutano, Serikali sasa imejikita pia katika kuimarisha utalii wa michezo kama bidhaa nyingine muhimu ya utalii.

Katika ziara hiyo, Crawford anatarajiwa kutembelea vivutio mbalimbali vya utalii ikiwemo Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro kwa lengo la kujionea vivutio vya Tanzania na kuvizungumza katika majukwaa ya kimataifa.

Akizungumzia ujio wake mwana masumbwi huyo ambaye ni raia wa Marekani amesema anafurahi kupata ziara ya wiki moja kujionea utalii na shughuli mbalimbali za michezo.

spot_img

Latest articles

Ofisi ya Msajili wa Hazina yatoa wito wa utawala bora kuimarisha uwekezaji wa umma

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH) imesisitiza kuwa mustakabali wa mafanikio...

DAWASA yasisitiza matumizi ya bidhaa za ndani kuimarisha huduma ya maji

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

DCEA yateketeza kilo 504.36 za Heroin Mtwara

Na Mwandishi Wetu, Mtwara MAMLAKa ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imeteketeza...

Mkurugenzi wa Rasilimali Watu Tanesco awahakikishia ushirikiano maafisa huduma kwa wateja

📌 Afunga Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa hao 📌 Awapongeza kwa utendaji bora wenye...

More like this

Ofisi ya Msajili wa Hazina yatoa wito wa utawala bora kuimarisha uwekezaji wa umma

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH) imesisitiza kuwa mustakabali wa mafanikio...

DAWASA yasisitiza matumizi ya bidhaa za ndani kuimarisha huduma ya maji

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

DCEA yateketeza kilo 504.36 za Heroin Mtwara

Na Mwandishi Wetu, Mtwara MAMLAKa ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imeteketeza...