Katibu Mkuu Maji aitaka DAWASA kufunga mkanda mapambano upotevu wa maji

Na Mwandishi wetu

BARAZA kuu la Wafanyakazi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es salaam (DAWASA) limekutana kujadili na kuweka mwelekeo wa vipaumbele vya Mamlaka kuelekea mwaka wa fedha 2026/2027, likilenga kuimarisha utoaji wa huduma ya majisafi na salama kwa wananchi.

Akizungumza katik kikao kazi hicho, Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Mhandisi Mwajuma Waziri, amesema Baraza la wafanyakazi ni jukwaa muhimu la mawasiliano linalowaunganisha Menejimenti na watumishi katika kupanga mikakati ya kuboresha huduma kwa wananchi.

“Niwashukuru kwa kunialika kuwa mgeni rasmi katika tukio hili. Ni matumaini yangu kuwa majadiliano yenu yatajikita katika kukabiliana na changamoto ya upotevu wa maji ili kuimarisha huduma na kuokoa mapato yanayopotea,” amesema Mhandisi Mwajuma.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa DAWASA, Mhandisi Romanus Mwangingo, amesema kipaumbele kikuu cha Mamlaka kwa sasa ni kukabiliana na changamoto ya upotevu wa maji, akibainisha kuwa tayari hatua mbalimbali zimeanza kuchukuliwa.

“Tunawekeza katika kupunguza upotevu wa maji kwa kununua mita za malipo ya kabla kwa ajili ya wateja na kubadilisha miundombinu chakavu ambayo imekuwa ikichangia upotevu huo,” amesema Mhandisi Mwangingo.

Naye Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA, Mhandisi Mkama Bwire, amewashukuru viongozi wa sekta ya maji kwa kushiriki katika uzinduzi wa kikao hicho, na kuwataka wajumbe wa Baraza la wafanyakazi kushirikiana kikamilifu katika utekelezaji wa maelekezo yaliyotolewa.

“Ni muhimu kila mmoja wetu akawa sehemu ya suluhisho kwa kutoa elimu kwa watumishi wenzake ili kusimama kwa pamoja katika kukabiliana na changamoto ya upotevu wa maji,” amesema Mhandisi Bwire.

spot_img

Latest articles

Sangweni: Sekta ya Mafuta na Gesi Ni Chachu ya Ukuaji wa Uchumi wa Taifa

Na Mwandishi Wetu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli...

VETA Kihonda yaja ‘cold room’ kupunguza upotevu wa mazao ya wakulima

Na Mwandishi Wetu UBUNIFU wa mfumo jumuishi wa kuhifadhi mazao kwa kutumia teknolojia ya ubaridi...

Ofisi ya Msajili wa Hazina yalenga kukusanya Sh2 trilioni mwaka 2026/27

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OTR) imejiwekea lengo la kukusanya Sh2...

MAULIDI KITENGE AUNGANA NA TANESCO KUHAMASISHA NISHATI SAFI YA KUPIKIA KWA UMEME

📌 Aahidi kutumia jukwaa lake kuhamasisha wananchi kutumia umeme kwa shughuli za kupikia 📌 Ushirikiano...

More like this

Sangweni: Sekta ya Mafuta na Gesi Ni Chachu ya Ukuaji wa Uchumi wa Taifa

Na Mwandishi Wetu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli...

VETA Kihonda yaja ‘cold room’ kupunguza upotevu wa mazao ya wakulima

Na Mwandishi Wetu UBUNIFU wa mfumo jumuishi wa kuhifadhi mazao kwa kutumia teknolojia ya ubaridi...

Ofisi ya Msajili wa Hazina yalenga kukusanya Sh2 trilioni mwaka 2026/27

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OTR) imejiwekea lengo la kukusanya Sh2...