Rais Samia akabidhi 94.1 bilioni mikopo ya wanawake, vijana

Na Mwandishi Wetu

SERIKALI imekabidhi hundi ya shilingi 94.1 bilioni kwa ajili ya mikopo ya wanawake, vijana, watu wenye ulemavu, wafanyabiashara wadogo, wakiwemo mamalishe na babalishe, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuwawezesha kukuza mitaji na kuimarisha shughuli zao za kiuchumi.

Hundi hiyo imekabidhiwa leo Jumanne Aprili 21, 2026 na Rais Samia Suluhu Hassan kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Tamisemi), Profesa Riziki Shemdoe, kwa niaba ya kundi hilo.

Katika kongamano hilo, Rais Samia pia ametunukiwa Tuzo ya Malkia wa Nishati Safi iliyotolewa na Umoja wa Mamalishe (Umalita), ikiwa ni kutambua mchango wake katika kuhamasisha matumizi ya nishati safi nchini.

Akizungumza katika kongamano hilo, Rais Samia amesema shughuli za Mama Lishe na Baba Lishe zinapaswa kutambuliwa na kuheshimiwa kutokana na mchango mkubwa wanaoutoa katika maisha ya kila siku ya Watanzania.

“Mtakubaliana nami kwamba shughuli za Mamalishe na Babalishe zinastahili kutambuliwa na kuheshimiwa kwa hadhi inayolingana na mchango wao katika maisha yetu ya kila siku. Yale yaliyosemwa hapa ya kunyanyaswa, ya kusumbuliwa, hayapaswi kufanywa kwa kundi hili,” amesema.

Amesema kuwa Serikali itaendelea kuweka mazingira rafiki yatakayowawezesha wafanyabiashara hao wadogo kufanya kazi zao kwa utulivu na usalama, huku akiwataka viongozi wa maeneo mbalimbali kuacha vitendo vya unyanyasaji dhidi yao.

spot_img

Latest articles

Sangweni: Sekta ya Mafuta na Gesi Ni Chachu ya Ukuaji wa Uchumi wa Taifa

Na Mwandishi Wetu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli...

VETA Kihonda yaja ‘cold room’ kupunguza upotevu wa mazao ya wakulima

Na Mwandishi Wetu UBUNIFU wa mfumo jumuishi wa kuhifadhi mazao kwa kutumia teknolojia ya ubaridi...

Ofisi ya Msajili wa Hazina yalenga kukusanya Sh2 trilioni mwaka 2026/27

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OTR) imejiwekea lengo la kukusanya Sh2...

MAULIDI KITENGE AUNGANA NA TANESCO KUHAMASISHA NISHATI SAFI YA KUPIKIA KWA UMEME

📌 Aahidi kutumia jukwaa lake kuhamasisha wananchi kutumia umeme kwa shughuli za kupikia 📌 Ushirikiano...

More like this

Sangweni: Sekta ya Mafuta na Gesi Ni Chachu ya Ukuaji wa Uchumi wa Taifa

Na Mwandishi Wetu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli...

VETA Kihonda yaja ‘cold room’ kupunguza upotevu wa mazao ya wakulima

Na Mwandishi Wetu UBUNIFU wa mfumo jumuishi wa kuhifadhi mazao kwa kutumia teknolojia ya ubaridi...

Ofisi ya Msajili wa Hazina yalenga kukusanya Sh2 trilioni mwaka 2026/27

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OTR) imejiwekea lengo la kukusanya Sh2...