Na Mwandishi Wetu
Mahakama ya Wilaya ya Kasulu imemhukumu mshitakiwa Nuru Hamimu Omary (48), mkulima na Mganga wa tiba asili, mkazi wa Kijiji cha Mwamgongo, Wilaya ya Kigoma kifungo cha kwenda jela miaka 30 baada ya kumtia hatiani kwa kosa la kumbaka mtoto wa kike mwenye umri wa miaka 12.
Mshtakiwa alitenda kosa hilo Septemba 28, 2025 huko Mtaa wa Murusi Wilayani Kasulu na kufikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza Oktoba 15, 2025.
Akitoa huku hiyo jana April 20, 2026 Hakimu Mkazi Mwandamizi, Immaculate Shuli amesema kuwa mahakama imejiridhisha pasipo na shaka ushahidi uliotolewa na upande wa mashtaka na hatimaye kumtia hatiani mshitakiwa kwa kosa hilo.
Mshitakiwa huyo amehukumiwa kifungo hicho ili iwe fundisho kwa wahalifu wanaojihusisha na vitendo vya ukiukaji wa sheria, maadili na ukatili wa kijinsia dhidi ya watoto.


