CRDB yaandika historia, yapata faida ya Trilioni 1

Na Mwandishi wetu

BENKI ya CRDB imepata faida ya Sh trilioni moja kabla ya kodi katika Kipindi cha mwaka 2025 ikiwa ni mara ya kwanza kuandika historia hiyo.

Akizungumza wakati wa sherehe za utoaji tuzo za CEO AWARDS zilizofanyika katika Ukumbi wa Super Dome Masaki jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dkt Abdulmajid Nsekela, amesema hatua hiyo imeifanya benki izidi kutambuliwa ndani na nje ya nchi na kutunukiwa tuzo nyingi kama vile kutambuliwa kuwa benki bora Tanzania, benki bora kwa wateja wadogo na wa Kati ambazo zinaenda sambamba na ubora wa wafanyakazi walionao.

Kwa upande wake Mwenyekiti Mstaafu wa Bodi ya Wakurugenzi CRDB, Dkt Ally Laay, amesema anajivunia utendaji uliotukuka wa Dkt Nsekela kutokana na mafanikio iliyopata benki hiyo kwa kipindi kifupi tangu achukue nafasi hiyo.

Amesema wakati Dkt Nsekela anachukua nafasi ya CEO hisa ilikiwa Sh 95 lakini hivi sasa imepanda na kufikia Sh 3,150 akisema hatua hiyo imetengeneza matajiri wengi kwa kupanda kwa bei ya hisa.

Tuzo hizo za heshima zinalenga kuwatambua wafanyakazi na idara zilizofanya vizuri na kuwapa motisha kuonyesha benki yao inawathamini.

spot_img

Latest articles

Latra yatangaza nauli mpya za mabasi, daladala

Na Mwandishi Wetu Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) imetoa bei mpya za nauli kwa...

Serikali yatoa neno vipaji vya kuogelea Afrika Mashariki vikichanua Dar

Na Winfrida Mtoi ​MASHINDANO ya kuogelea kwa watoto ya ‘East Africa Development Swimming Gala’ yameanza...

Simba yapewa wakusanya kodi, Yanga maafande

Na Mwandishi Wetu DROO ya hatua ya robo fainali ya michuano ya Kombe la Shirikisho,...

Waziri Mkuu ahimiza ufungaji kamera  viwanjani kudhibiti ushirikina

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk.Mwigulu Nchemba, amehimiza ufungaji wa kamera nyingi katika viwanja vya...

More like this

Latra yatangaza nauli mpya za mabasi, daladala

Na Mwandishi Wetu Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) imetoa bei mpya za nauli kwa...

Serikali yatoa neno vipaji vya kuogelea Afrika Mashariki vikichanua Dar

Na Winfrida Mtoi ​MASHINDANO ya kuogelea kwa watoto ya ‘East Africa Development Swimming Gala’ yameanza...

Simba yapewa wakusanya kodi, Yanga maafande

Na Mwandishi Wetu DROO ya hatua ya robo fainali ya michuano ya Kombe la Shirikisho,...