Waziri Sangu aongoza maadhimisho ya miaka 19 ya Kanisa la WRC

Na Mwandishi Wetu

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Deus Sangu ameongoza maadhimisho ya miaka 19 ya Kanisa la Huduma ya Neno la Upatanisho (WRC), linaloongozwa na Askofu na Nabii Nicolaus Suguye.

Katika maadhimisho hayo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam, Waziri Sangu aliambatana na Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Edward Mpogolo, Mbunge wa Kivule, Ojambi Massaburi pamoja na Mbunge wa Bunda, Ester Bulaya, ambapo walipokelewa na waumini na viongozi wa kanisa hilo.

Mbali na viongozi hao, pia walihudhuria viongozi mbalimbali wa dini akiwemo Askofu wa Kanisa la Arise & Shine, Boniphace Mwamposa na Askofu wa Kanisa la Ufunuo Tanzania, Paul Bendera.

Maadhimisho hayo yalipambwa na nyimbo za sifa na shukrani, huku waumini wakionesha furaha na kujivunia mafanikio ya kanisa lao tangu kuanzishwa kwake.

Akizungumza katika hafla hiyo, Waziri Sangu alipongeza huduma inayotolewa na kanisa hilo, akisema imekuwa na mchango mkubwa kwa jamii.

“Tunafurahia kazi ya Mungu mnayoifanya kupitia huduma yenu. Heshima hii umepewa Askofu kwa kazi kubwa uliyoifanya,” amesema.

Waziri Sangu amesisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya serikali na taasisi za dini katika kuimarisha maendeleo ya jamii na kudumisha amani nchini.

Amesema taasisi za dini zimekuwa na mchango mkubwa katika malezi ya maadili pamoja na utoaji wa huduma kwa jamii.

Aidha, amewasilisha salamu kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, akibainisha kuwa serikali inaendelea kuthamini mchango wa taasisi hizo katika kuleta mshikamano na maendeleo.

Ameongeza kuwa katika miaka ya hivi karibuni, taasisi za dini zimekuwa mstari wa mbele kusaidia jamii kwa kutoa misaada kwa wahitaji na kushiriki katika shughuli mbalimbali za kijamii.

Waziri huyo pia ameahidi kuwa serikali itaendelea kushirikiana kwa karibu na taasisi hizo ili kuhakikisha huduma bora zinawafikia wananchi pamoja na kutatua changamoto zinazowakabili.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Mpogolo, akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila amewashukuru viongozi wa dini kwa mchango wao mkubwa katika kudumisha amani na utulivu mkoani Dar es Salaam.

“Tuna kila sababu ya kuwashukuru na kumtukuza Mungu. Hata tulipowahitaji walikuja bila kusita. Mafanikio na utulivu tunaouona leo ni matokeo ya mchango mkubwa wa viongozi wa dini, ambao ni muhimu sana katika mkoa huu.” amesema.

spot_img

Latest articles

TPDC Yahimiza Wananchi Kulinda Miundombinu ya Bomba la Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu SHIRIKA la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) limeendelea kuwashirikisha wananchi...

TMA yatangaza msimu wa Kipupwe Juni hadi Agosti

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetangaza kuwa na msimu...

Kamati ya Bunge yaridhishwa na uzalishaji wa kiwanda cha sukari Mkulazi

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imeendelea kutekeleza mikakati iliyoanishwa katika Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050...

Wachina wanne wakamatwa kwa utekaji

Na Mwandishi Wetu JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linawashikilia raia wanne...

More like this

TPDC Yahimiza Wananchi Kulinda Miundombinu ya Bomba la Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu SHIRIKA la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) limeendelea kuwashirikisha wananchi...

TMA yatangaza msimu wa Kipupwe Juni hadi Agosti

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetangaza kuwa na msimu...

Kamati ya Bunge yaridhishwa na uzalishaji wa kiwanda cha sukari Mkulazi

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imeendelea kutekeleza mikakati iliyoanishwa katika Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050...