Na Mwandishi wetu
Watanzania wameaswa kudumisha amani na mshikamano kuelekea sikukuu ya pasaka ili kuupokea ufufuko wa yesu kristu kwa roho na kweli.
Wakati akitoa salamu za pasaka Askofu wa kanisa la WRC ( The word ofvReconciliation church) Askofu Nicklous Suguye amesema kuwa watanzania ni watu wenye utamaduni wa upole na kupenda amani.
Aidha ameongeza kwa kusema kuwa kama nchi tunapashwa kuwa wamoja bila kujali itikadi za kidini, kisiasa na kikabila ili kuijenga nchi iliyo na umojaLakini pia amewataka waamini kujiungamanisha na yesu kristu kwa siku zilizo baki kuanzia leo ijumaa kuu mpaka kufikia pasaka ufufuko wa yesu kristuJumatatu ya pasaka itakuwa ni siku ya maadhimisho ya miaka 19 ya kanisa la WRC ( The word of Reconciliation Church) na kuwakaribisha Watanzania wote kushiriki kwa pamoja kumtukuza Mungu.


