Mwili wa Mwanahabari Mkongwe Makaranga waagwa Dar, kuzikwa Mwanza

Na Mwandishi Wetu

WAANDISHI wa Habari, Wahariri, ndugu na jamaa leo Machi 10, 2026, wamejumuika pamoja katika ibada ya kuaga mwili wa Mhariri Mkongwe, Revocatus Makaranga iliyofanyika kwenye Kanisa Katoliki Parokia ya Kimara, Dar es Salaam.

Makaranga ambaye amewahi kufanya kazi na vyombo vya mbalimbali vya habari nchini, alifariki usiku wa kuamkia Machi 5, 2025, katika Hospitali ya Taifa Muhimbili alikopelekwa kwa ajili ya matibabu.

Baada ya ibada ya kutoa heshima za mwisho, mwili wa marehemu umesafirishwa kwenda jijini Mwanza kwa ajili ya mazishi yanayotarajiwa kufanyika kesho.

Marehemu ni mmoja wa waandishi na wahariri wakongwe nchini waliotoa mchango mkubwa katika tasnia ya habari, akifanya kazi katika vyombo vya habari vya umma wakati wa mfumo wa chama kimoja na baadaye vyama vingi, pia alifanya kazi katika kampuni binafsi za Mwananchi Communications Ltd (MCL), New Habari Ltd.

Makaranga ni mhitimu wa shahada ya uzamili katika uandishi wa habari kutoka Chuo Kikuu cha Cardiff, Wales, Uingereza.

spot_img

Latest articles

Mkurugenzi wa Rasilimali Watu Tanesco awahakikishia ushirikiano maafisa huduma kwa wateja

📌 Afunga Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa hao 📌 Awapongeza kwa utendaji bora wenye...

Makonda  awajibu wanaoponda ziara ya Rio

Na Winfrida Mtoi WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amesema ziara ya...

TIRDO yasajili Viwanda 25,650, Yaongeza Maabara za Kisasa Kuimarisha Sekta ya Viwanda

Na Mwandishi Wetu WIZARA ya Viwanda na Biashara kupitia Shirika la Utafiti na Maendeleo ya...

MD Twange aeleza kutoridhishwa na kasi ya Mkandarasi wa mradi wa Hale

📍Ni ule wa kuboresha kituo cha kufua umeme 📍Amuagiza kuongeza kasi ya utekelezaji wa...

More like this

Mkurugenzi wa Rasilimali Watu Tanesco awahakikishia ushirikiano maafisa huduma kwa wateja

📌 Afunga Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa hao 📌 Awapongeza kwa utendaji bora wenye...

Makonda  awajibu wanaoponda ziara ya Rio

Na Winfrida Mtoi WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amesema ziara ya...

TIRDO yasajili Viwanda 25,650, Yaongeza Maabara za Kisasa Kuimarisha Sekta ya Viwanda

Na Mwandishi Wetu WIZARA ya Viwanda na Biashara kupitia Shirika la Utafiti na Maendeleo ya...