ETDCO yaahidi kukamilisha Mradi wa Umeme katika vitongoji 372 Ruvuma kwa wakati

Na Mwandishi Wetu

KAMPUNI ya Ujenzi na Ukarabati wa Miundombinu ya Usafirishaji na Usambazaji wa Umeme (ETDCO) imeahidi kukamilisha kwa wakati mradi wa kusambaza umeme katika vitongoji 372 wenye thamani ya shilingi bilioni 37.9, Mkoani Ruvuma.

Akizungumza katika hafla ya makabidhiano ya utekelezaji wa mradi huo kati ya ETDCO na Wakala wa Nishati Vijijini (REA), iliyofanyika Februari 3, 2026 Mkoani Ruvuma, Mkuu wa Mkoa huo, Brigedia Jenerali Ahmed Ahmed, ameitaka Kampuni ya ETDCO kuhakikisha mradi huo unakamilika kwa wakati katika wilaya za Mbinga na Nyasa.

Brigedia Jenerali Ahmed, amesema kuwa kukamilika kwa mradi huo kutachochea shughuli za maendeleo ya kijamii na kiuchumi katika Mkoa huo, huku akiwahimiza wananchi kujiandaa kuweka miundombinu ya umeme majumbani (wiring) ili waweze kuunganishwa na huduma hiyo mara baada ya mradi kukamilika.

“Ujio wa umeme huo utasaidia kukuza shughuli za kiuchumi na biashara katika maeneo husika,” amesema Kanali Ahmed.

Meneja Usamamizi wa Miradi ya Kusambaza Umeme REA, Mhandisi Deogratius Nagu, amesema kuwa mradi huo unatarajiwa kuwanufaisha wateja takribani 11,914 katika Wilaya za Mbinga na Nyasa.

Kwa upande wake, Kaimu Meneja Mkuu wa ETDCO, Mhandisi Richard Mwanja, ameishukuru Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kuipa ETDCO fursa ya kutekeleza mradi huo, huku akieleza kuwa Kampuni hiyo imejipanga kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati uliopangwa.

Msimamizi wa Mradi kutoka Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Mkoa wa Ruvuma, Mhandisi Ali Pandit, amesema kuwa TANESCO imejipanga kuhakikisha miradi inakamilika kwa wakati ili huduma ya umeme inawafikia wananchi.

Kwa upande wao, Wananchi wa Mkoa wa Ruvuma wameipongeza Serikali kupitia REA kwa kuwaletea miradi ya kusambaza umeme katika vitongoji vyao, wakisema kuwa miradi hiyo itasaidia kuleta maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

spot_img

Latest articles

TTB yakutanisha wadau kujadili mustakabali wa Destination Tanzania

Na Mwandishi Wetu Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imewakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya...

Sangweni: Sekta ya Mafuta na Gesi Ni Chachu ya Ukuaji wa Uchumi wa Taifa

Na Mwandishi Wetu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli...

VETA Kihonda yaja ‘cold room’ kupunguza upotevu wa mazao ya wakulima

Na Mwandishi Wetu UBUNIFU wa mfumo jumuishi wa kuhifadhi mazao kwa kutumia teknolojia ya ubaridi...

Ofisi ya Msajili wa Hazina yalenga kukusanya Sh2 trilioni mwaka 2026/27

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OTR) imejiwekea lengo la kukusanya Sh2...

More like this

TTB yakutanisha wadau kujadili mustakabali wa Destination Tanzania

Na Mwandishi Wetu Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imewakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya...

Sangweni: Sekta ya Mafuta na Gesi Ni Chachu ya Ukuaji wa Uchumi wa Taifa

Na Mwandishi Wetu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli...

VETA Kihonda yaja ‘cold room’ kupunguza upotevu wa mazao ya wakulima

Na Mwandishi Wetu UBUNIFU wa mfumo jumuishi wa kuhifadhi mazao kwa kutumia teknolojia ya ubaridi...