Wawili wajeruhiwa ajali ya moto Dar

Na Mwandishi Wetu

WATU wawili wamejeruhiwa kutokana na ajali ya moto iliyotokea leo Januari 16,2025 katika jengo la NSSF lililopo katika mtaa wa Azikiwe na Samora, Posta,Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya zoezi la uokoaji Mkaguzi Msaidizi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Ilala, Frank Mwalongo amethibitisha kujeruhiwa kwa watu  hao wawili ambao wamewahishwa hospitali ya Mnazi Mmoja kwa huduma ya kwanza.

“Majira ya saa sita na robo mchana tulipokea wito wa dharura kuhusu ajali ya moto katika jengo la NSSF, na walifanikiwa kufika eneo la tukio kwa wakati na kuweza kupambana na moto huo na kuudhibiti,” amesema.

Ameeleza kuwa ajali hiyo haijaleta madhara makubwa kwa jengo ambapo ghrofa  ya kwanza ya jingo ndiyo imeathirika kidogo, lakini mali zimeokolewa na watu wote walikuwemo ndani wako salama.

Mwalongo amesema bado chanzo cha moto huo hakijajulikana, uchunguzi  unaendelea na ukikamilika taarifa rasmi itatolewa.

spot_img

Latest articles

Mkurugenzi wa Rasilimali Watu Tanesco awahakikishia ushirikiano maafisa huduma kwa wateja

📌 Afunga Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa hao 📌 Awapongeza kwa utendaji bora wenye...

Makonda  awajibu wanaoponda ziara ya Rio

Na Winfrida Mtoi WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amesema ziara ya...

TIRDO yasajili Viwanda 25,650, Yaongeza Maabara za Kisasa Kuimarisha Sekta ya Viwanda

Na Mwandishi Wetu WIZARA ya Viwanda na Biashara kupitia Shirika la Utafiti na Maendeleo ya...

MD Twange aeleza kutoridhishwa na kasi ya Mkandarasi wa mradi wa Hale

📍Ni ule wa kuboresha kituo cha kufua umeme 📍Amuagiza kuongeza kasi ya utekelezaji wa...

More like this

Mkurugenzi wa Rasilimali Watu Tanesco awahakikishia ushirikiano maafisa huduma kwa wateja

📌 Afunga Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa hao 📌 Awapongeza kwa utendaji bora wenye...

Makonda  awajibu wanaoponda ziara ya Rio

Na Winfrida Mtoi WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amesema ziara ya...

TIRDO yasajili Viwanda 25,650, Yaongeza Maabara za Kisasa Kuimarisha Sekta ya Viwanda

Na Mwandishi Wetu WIZARA ya Viwanda na Biashara kupitia Shirika la Utafiti na Maendeleo ya...