Warning: Array to string conversion in /home/themedia/domains/themediabrains.com/public_html/wp-includes/shortcodes.php on line 434
Array

Familia yaondoa vitu nyumbani kwa Polepole

Na Mwandishi Wetu

FAMILIA ya aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Cuba, Humphrey Polepole, leo Jumanne, Januari 6, 2026, imefika katika nyumba aliyokuwa akiishi eneo la Ununio jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kukusanya mali zake, pamoja na kufanya maombi kwenye nyumba aliyokuwa akiishi.

Ndugu hao wakiongozwa na mama mzazi wa Humphrey Polepole, Mama Anna Marry Polepole na mdogo wake Godfrey Polepole, wamesema wataendelea kumuombea ndugu yao na kuisihi jamii kuendelea kushirikiana na vyombo husika pale taarifa zozote zitakapopatikana

Akizungumza na waandishi wa habari, Mama wa Polepole ameeleza kuwa wamekwenda kutoa vitu katika nyumba hiyo aliyokuwa amepanda mwanaye kwa sababu hakuna anayeweza kulipa kodi.

Amesisitiza kuwa anaomba waliomchukua mtoto wake wamrudishe akiwa mzima  na ikiwa ana makosa aliyofanya  ashtakiwe kama wengine.

Polepole, ambaye aliwahi kushika nyadhifa mbalimbali serikalini alidaiwa kutekwa na watu wasiojulikana miezi mitatu iliyopita na hadi sasa hatima yake ikiwa bado haijulikani rasmi.

spot_img

Latest articles

Kamati ya kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini yaipongeza Tanesco utekelezaji wa Mradi wa Umeme Jua Kishapu

📌 Watembelea mradi kuona ufanisi wake 📌 Shilingi bilioni 118 zatumika kutekeleza mradi 📌 Watoa rai...

Kamati ya kudumu ya Binge Nishati na Madini yaridhishwa na maendeleo ya Kiwanda cha nguzo za zege

📌Ni mradi wa kihistoria kutekelezwa chini ya Serikali ya awamu ya Sita 📌 Yaipongeza...

Waziri Ulega, RC Chalamila pekueni mafaili wizarani

KWA nyakati tofauti viongozi wawili wamezungumzia jiji la Dar es Salaam kuhusu msongamano wa...

Rais Samia amuasili mtoto mchanga aliyetelekezwa Nzega

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ,Samia Suluhu Hassan, amemuasili mtoto...

More like this

Kamati ya kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini yaipongeza Tanesco utekelezaji wa Mradi wa Umeme Jua Kishapu

📌 Watembelea mradi kuona ufanisi wake 📌 Shilingi bilioni 118 zatumika kutekeleza mradi 📌 Watoa rai...

Kamati ya kudumu ya Binge Nishati na Madini yaridhishwa na maendeleo ya Kiwanda cha nguzo za zege

📌Ni mradi wa kihistoria kutekelezwa chini ya Serikali ya awamu ya Sita 📌 Yaipongeza...

Waziri Ulega, RC Chalamila pekueni mafaili wizarani

KWA nyakati tofauti viongozi wawili wamezungumzia jiji la Dar es Salaam kuhusu msongamano wa...