Balozi Bandora kuzikwa kesho makaburi ya Kinondoni

Mwanadiplomasia nguli wa Tanzania, aliyewahi  kuwa Balozi wa Tanzania nchini Nigeria na Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Eswatini na Namibia, Timothy Bandora (72),  anatarajia kuzikwa kesho Desemba 16, 2025, katika Makaburi ya Kinondoni.

 Balozi  Bandora alifariki dunia  wiki iliyopita   akiwa jijini Nairobi, nchini Kenya, ambako alikuwa akipatiwa matibabu.

Aliitumikia Serikali kuanzia awamu ya kwanza hadi ya tatu, alitekeleza majukumu mbalimbali ya kitaifa na kimataifa katika utumishi wa umma pamoja na ndani ya Umoja wa Mataifa (UN), akihudumu katika nyadhifa tofauti kwa uadilifu na weledi mkubwa.

Kwa mujibu wa ratiba ya msiba iliyotolewa na familia, ibada ya mazishi itafanyika katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Msasani, jijini Dar es Salaam.

Miongoni mwa majukumu aliyofanya wakati wa uhai wake ni kuongoza kurugenzi ya ushirikiano wa kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje, Balozi wa Tanzania nchini Nigeria ofisi ya Lagos, ambayo pia inahudumia nchi za Benin, Togo, Cote d’Ivoire, Ghana, Guinea, Senegal, Burkina Faso, Mali, Sierra Leone, Liberia, Guinea-Bissau na Mauritania.

spot_img

Latest articles

Dk. Mwigulu: Tutamuenzi kwa vitendo marehemu Jenista

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itayaendeleza mambo yote mema yaliyofanywa na...

Serikali yajipanga kuimarisha utumishi wa umma, kuendeleza mageuzi ya kidigitali

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa...

Bokya amtahadharisha mapema Tyson wa Bongo

Na Winfrida Mtoi Bondia Ismail Khalid maarufu Boyka ametamba kutoa kipigo kikali kwa mpinza wake...

Mwili wa Jenista Mhagama Kuzikwa Jumanne Mbinga, Ruvuma

Na Mwandishi Wetu MWILI wa aliyekuwa Mbunge wa Peramiho (CCM), Jenista Mhagama unatarajiwa kuzikwa...

More like this

Dk. Mwigulu: Tutamuenzi kwa vitendo marehemu Jenista

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itayaendeleza mambo yote mema yaliyofanywa na...

Serikali yajipanga kuimarisha utumishi wa umma, kuendeleza mageuzi ya kidigitali

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa...

Bokya amtahadharisha mapema Tyson wa Bongo

Na Winfrida Mtoi Bondia Ismail Khalid maarufu Boyka ametamba kutoa kipigo kikali kwa mpinza wake...