Serikali yawaita wadau kujitokeza kusapoti ushiriki wa wanawake michezoni

Na Winfrida Mtoi

Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma ‘MwanaFA’ amewaomba wadau na wadhamini kujitokeza kusapoti ushiriki wa wanawake katika michezo ili kuweka uwiano sawa na wanaume.

Amesema ushiriki wa wanawake katika riadha kwa Tanzania bado ni mdogo ukilinganisha na wanaume, hali inayochangiwa na majukumu mengi kwa mwanamke.

Amezungumza hayo wakati wa ufunguzi wa mashindano ya riadha kwa wanawake maafuru Ladies First, yanayofanyika kwenye Uwanja wa Mkapa, jijini Dar es Salaam.

MwanaFA amesema kuna ni muhimu kuungana pamoja kuhakikisha dhana potofu inayozuia wanawake kushiriki michezo inaondolewa, huku akisisitiza kufanyika kwa mashindano mengi yanayoshirikisha wanawake.

Naibu waziri huyo ameeleza kuwa jamii inatakiwa kutambua kuwa kwa michezo ni ajira, inakuza uchumi na Serikali ina matumaini makubwa ya vipaji vipya vinavyoibuliwa kupitia mashindano hayo.

Akizungumzia Ladies First ameleza kuwa, mashindano hayo yamekuwa katika kuandaa wanariadha watakaoiwakilisha nchi katika mashindano mbalimbali ikiwamo ya Kimataifa.

“Niwapongeze sana JICA, Baraza la Michezo la Taifa (BMT) na Shirikisho la Riadha Tanzania (RT) kwa kuendesha mashindano haya kwa mafanikio makubwa. Yamekuwa yakifanyika kwa msimu wa saba sasa,” amesema.

Kwa upande wake Katibu Mtendaji wa BMT, Neema Msitha ameeleza kuwa heshima kubwa anampa muasisi wa mashindano hayo, mwanariadha mkongwe Kanali Mstaafu Juma Ikangaa kutokana na kuona umuhimu wa kuwapa nafasi wanawake kushiriki riadha.

spot_img

Latest articles

ETDCO yaahidi kukamilisha Mradi wa Umeme katika vitongoji 372 Ruvuma kwa wakati

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI ya Ujenzi na Ukarabati wa Miundombinu ya Usafirishaji na Usambazaji...

Wadau sekta ya Hali ya Hewa wajadili utabiri wa Masika 2026

Na Mwandishi Wetu WADAU kutoka sekta mbalimbali nchini wamekutana kujadili utabiri wa msimu wa...

WMA yafunga Mtambo wa kisasa unaohakiki Dira za Maji Dodoma

Na Mwandishi Wetu WAKALA wa Vipimo (WMA) umesimika mtambo wa kisasa wa kidijitali wa...

Benki ya CRDB yaja na ‘Benki Kimpango Wako’ yaahidi huduma bora zaidi mwaka 2026

Na Mwandishi wetu BENKI ya CRDB imezindua kampeni yake ya mwaka 2026 inayoitwa ‘Benki Kimpango...

More like this

ETDCO yaahidi kukamilisha Mradi wa Umeme katika vitongoji 372 Ruvuma kwa wakati

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI ya Ujenzi na Ukarabati wa Miundombinu ya Usafirishaji na Usambazaji...

Wadau sekta ya Hali ya Hewa wajadili utabiri wa Masika 2026

Na Mwandishi Wetu WADAU kutoka sekta mbalimbali nchini wamekutana kujadili utabiri wa msimu wa...

WMA yafunga Mtambo wa kisasa unaohakiki Dira za Maji Dodoma

Na Mwandishi Wetu WAKALA wa Vipimo (WMA) umesimika mtambo wa kisasa wa kidijitali wa...