Tume kuundwa kuchunguza vurugu zilizotokea Oktoba 29, mwaka huu

Na Mwandishi Wetu 

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametangaza kuundwa kwa Tume Maalumu ya Kuchunguza vurugu na ghasia zilizotokea Oktoba 29, 2025 wakati wa Uchaguzi Mkuu.

Akitangaza uamuzi huo wakati wa hotuba ya ufunguzi wa Bunge la 13 leo Novemba 14, 2025 jijini Dodoma, Rais Samia amesema Tume hiyo inalenga kubaini chanzo cha tukio hilo na kuishauri Serikali katika hatua za kurejesha amani na maridhiano.

“Serikali imechukua hatua ya kuunda Tume ya kuchunguza yaliyotokea ili tujue kiini cha tatizo. Taarifa hiyo itatuongoza kujielekeza kwenye mazungumzo ya kuleta maelewano na amani,” amesema.

Kabla ya kuendelea na hotuba yake, Rais Samia aliwaongoza Wabunge na wageni waalikwa kusimama kwa dakika moja kuwaombea wananchi waliopoteza maisha katika ghasia hizo na kutoa pole kwa familia zilizopoteza wapendwa wao pamoja na kuwaombea majeruhi kupona haraka. 

Aidha Rais Samia amevielekeza vyombo vya dola kuwasamehe wale wote walioshiriki katika vurugu za Oktoba 29 kwa kufuata mkumbo.

“Kuna wakati vijana hufuata mkumbo wa uhalifu kwa ushabiki. Natambua vijana wengi waliokamatwa hawakujua wanachofanya. Ninaviagiza vyombo vya sheria, hasa Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka, kuwatizama vijana waliofuata mkumbo na hawakudhamiria waweze kuwaachia,” amesema Rais Samia.

Mwisho 

spot_img

Latest articles

Mkakati wa Mawasiliano wa Nishati Safi ya kupikia: Dira ya Mafanikio ya Taifa

Na Mwandishi Wetu IMEELEZWA kuwa Mkakati wa Mawasiliano wa Nishati Safi ya Kupikia ni...

JKT Queens na matumaini nusu  fainali CAFWCL mbele ya TP Mazembe

Na Mwandishi Wetu Baada ya timu ya JKT Queens kutoa sare mbili mfululizo Ligi ya...

Rais Mwinyi ateua Mawaziri 20

Na Mwandishi Wetu Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali...

Mwigulu Waziri Mkuu wa Tanzania

Na Mwandishi Wetu Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limemthibitisha Dk. Mwigulu Nchemba, kuwa...

More like this

Mkakati wa Mawasiliano wa Nishati Safi ya kupikia: Dira ya Mafanikio ya Taifa

Na Mwandishi Wetu IMEELEZWA kuwa Mkakati wa Mawasiliano wa Nishati Safi ya Kupikia ni...

JKT Queens na matumaini nusu  fainali CAFWCL mbele ya TP Mazembe

Na Mwandishi Wetu Baada ya timu ya JKT Queens kutoa sare mbili mfululizo Ligi ya...

Rais Mwinyi ateua Mawaziri 20

Na Mwandishi Wetu Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali...