Bulugu awahamasisha Wafanyakazi Kiwanda cha Kahawa Mbozi kumpigia kura Dkt. Samia

Na Mwandishi Wetu

KATIBU Msaidizi Mkuu Idara ya Uhamasishaji na Chipukizi wa CCM, Bulugu Magege, leo 30/09/2025 amekutana na wafanyakazi wa Mbozi Coffee Curing Company Limited na kuwasisitiza wajibu wao wa kizalendo wa kumpa kura za kishindo Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na wagombea wa CCM katika nafasi za Ubunge na Udiwani.

Katika mazungumzo hayo, Bulugu aliwaeleza kuwa Dkt. Samia ni Kiongozi mwenye upendo na watanzania anayejali wakulima na wafanyakazi kwa kuendeleza sekta ya kilimo na viwanda hususani kahawa, ambayo ni uti wa mgongo wa wananchi wa Mbozi na mkoa mzima wa Songwe. Alisisitiza kuwa kura zao kwa Dkt. Samia ni kura za maendeleo ya kweli kwa taifa.

Katika ziara hiyo, Bulugu aliambatana na Haji Shabani Mwalimu, Katibu wa UVCCM Wilaya ya Mbozi na Noel Donald Mkwemba, Katibu wa Uhamasishaji na Chipukizi Mkoa wa Songwe.

Wote kwa pamoja waliwaeleza wafanyakazi hao kuwa CCM ni chombo pekee cha kuwaletea mustakabali bora na kuwataka watimize ahadi yao ya kumpa ushindi wa kishindo Dkt. Samia ifikapo Oktoba 29, 2025.

spot_img

Latest articles

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

Viongozi wa dini waendelea kihimiza amani uchaguzi mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam VIONGOZI wa dini nchini wameendelea kuhimiza umuhimu wa kudumisha...

Ujumbe wa viongozi wa dini kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 29, 2025 katika Kongamano la Kamati ya Amani Kitaifa Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu Askofu Mkuu Wapo Mission, Dk. Sylvester Gamanywa “Mungu ambaye tunamwakilisha ndiye anayweka watawala...

Watumishi wa umma waaswa kushiriki Uchaguzi wa Oktoba 29

Dar es Salaam. Ofisi ya Msajili wa Hazina (OMH) imetoa wito kwa watumishi wote...

More like this

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

Viongozi wa dini waendelea kihimiza amani uchaguzi mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam VIONGOZI wa dini nchini wameendelea kuhimiza umuhimu wa kudumisha...

Ujumbe wa viongozi wa dini kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 29, 2025 katika Kongamano la Kamati ya Amani Kitaifa Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu Askofu Mkuu Wapo Mission, Dk. Sylvester Gamanywa “Mungu ambaye tunamwakilisha ndiye anayweka watawala...