Timu ya Taifa kriketi ya wanawake kusaka tiketi ya kucheza Kombe la Dunia

Na Mwandishi Wetu

Timu ya Taifa ya wanawake ya mchezo wa kriketi ya Tanzania inatarajiwa kushiriki mashindano ya kufuzu Kombe la Dunia yatakayofanyika nchini Namibia kuanzia Agosti 30 hadi 5 Septemba 2025.

Mashindano hayo yanatarajiwa kushirikisha nchi nane kutoka Kanda ya Afrika ambazo ni Nigeria, Namibia, Kenya, Rwanda, Tanzania, Botswana na Uganda, ambazo zitachuana kuwania nafasi ya hatua za juu.

Kwa mujibu wa Shirikisho la Kriketi Tanzania (TCA), kikosi cha Tanzania kimejiandaa vyema na kipo tayari kwa ushindani mkubwa ili kuhakikisha kinapata nafasi ya kuiwakilisha nchi katika hatua zinazofuata za michuano ya dunia.

Wachezaji wa kikosi hicho wametoa wito kwa watanzania kuwapa sapoti ya hali na mali, wakibainisha kuwa uwepo wa mashabiki na hamasa kutoka nyumbani utawapa nguvu zaidi ya kupambana uwanjani.

Mashindano hayo yanachukuliwa kuwa hatua muhimu katika kuendeleza mchezo wa kriketi barani Afrika na kutoa nafasi kwa wachezaji chipukizi kuonyesha vipaji vyao, huku Tanzania ikitarajia kutumia mashindano haya kuinua hadhi ya mchezo huo nchini.

spot_img

Latest articles

Ndejembi ataka Ewura kukagua maghala ya mafuta kuhakikisha hakuna mafuta yanayofichwa

📌Asema nchi ina usalama mkubwa wa mafuta hivyo wananchi waendelee kupata huduma muda wote 📌Timu...

Tanesco yagusa mioyo ya watoto wenye mahitaji maalum

📌Ni sehemu ya uwajibikaji wake kwa jamii 📌Yatoa misaada mbalimbali kwa vituo vitatu Dar...

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

More like this

Ndejembi ataka Ewura kukagua maghala ya mafuta kuhakikisha hakuna mafuta yanayofichwa

📌Asema nchi ina usalama mkubwa wa mafuta hivyo wananchi waendelee kupata huduma muda wote 📌Timu...

Tanesco yagusa mioyo ya watoto wenye mahitaji maalum

📌Ni sehemu ya uwajibikaji wake kwa jamii 📌Yatoa misaada mbalimbali kwa vituo vitatu Dar...

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...