Timu ya Taifa kriketi ya wanawake kusaka tiketi ya kucheza Kombe la Dunia

Na Mwandishi Wetu

Timu ya Taifa ya wanawake ya mchezo wa kriketi ya Tanzania inatarajiwa kushiriki mashindano ya kufuzu Kombe la Dunia yatakayofanyika nchini Namibia kuanzia Agosti 30 hadi 5 Septemba 2025.

Mashindano hayo yanatarajiwa kushirikisha nchi nane kutoka Kanda ya Afrika ambazo ni Nigeria, Namibia, Kenya, Rwanda, Tanzania, Botswana na Uganda, ambazo zitachuana kuwania nafasi ya hatua za juu.

Kwa mujibu wa Shirikisho la Kriketi Tanzania (TCA), kikosi cha Tanzania kimejiandaa vyema na kipo tayari kwa ushindani mkubwa ili kuhakikisha kinapata nafasi ya kuiwakilisha nchi katika hatua zinazofuata za michuano ya dunia.

Wachezaji wa kikosi hicho wametoa wito kwa watanzania kuwapa sapoti ya hali na mali, wakibainisha kuwa uwepo wa mashabiki na hamasa kutoka nyumbani utawapa nguvu zaidi ya kupambana uwanjani.

Mashindano hayo yanachukuliwa kuwa hatua muhimu katika kuendeleza mchezo wa kriketi barani Afrika na kutoa nafasi kwa wachezaji chipukizi kuonyesha vipaji vyao, huku Tanzania ikitarajia kutumia mashindano haya kuinua hadhi ya mchezo huo nchini.

spot_img

Latest articles

Ofisi ya Msajili wa Hazina yatoa wito wa utawala bora kuimarisha uwekezaji wa umma

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH) imesisitiza kuwa mustakabali wa mafanikio...

TTB yamkaribisha bingwa wa Masumbwi duniani Terence kwa ziara ya utalii

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Ephraim Mafuru, amemkaribisha nchini...

DAWASA yasisitiza matumizi ya bidhaa za ndani kuimarisha huduma ya maji

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

DCEA yateketeza kilo 504.36 za Heroin Mtwara

Na Mwandishi Wetu, Mtwara MAMLAKa ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imeteketeza...

More like this

Ofisi ya Msajili wa Hazina yatoa wito wa utawala bora kuimarisha uwekezaji wa umma

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH) imesisitiza kuwa mustakabali wa mafanikio...

TTB yamkaribisha bingwa wa Masumbwi duniani Terence kwa ziara ya utalii

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Ephraim Mafuru, amemkaribisha nchini...

DAWASA yasisitiza matumizi ya bidhaa za ndani kuimarisha huduma ya maji

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...