Geofrey Timothy achukua fomu ya kugombea Ubunge Jimbo la Kawe

Na Mwandishi Wetu

MGOMBEA Ubunge wa Jimbo la Kawe kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Geofrey Timothy, amechukua fomu ya kuwania nafasi hiyo na kuahidi kuwatumikia wananchi wa Kawe kwa ari na moyo wa kujituma.

Akizungumza leo Agosti 26, 2025 mara baada ya kuchukua fomu, Timothy ameishukuru CCM kwa imani waliyoonesha kwake kwa kumteua kupeperusha bendera ya chama hicho katika uchaguzi wa mwaka huu.

“Nashukuru viongozi wa Chama kwa kuniteua kupeperusha bendera ya chama kupitia Jimbo la Kawe. Yapo mengi tumepanga kuyafanya…nawashukuru wajumbe kwa kunipigia kura nyingi kupeperusha bendera ya chama,” amesema.

Aidha, Timothy amewataka wakazi wa Kawe kujitokeza kwa wingi katika uzinduzi wa kampeni za CCM utakaofanyika Agosti 28, 2025, akisema utakuwa ni fursa ya wananchi kusikia kwa kina mipango ya chama na kuunga mkono jitihada za Rais Samia Suluhu Hassan.

Amesema Chama hicho kimejipanga kwa mikakati thabiti ya kuendeleza utekelezaji wa Ilani kwa vitendo, ikiwemo kuboresha huduma za kijamii, kuongeza ajira kwa vijana pamoja na kukuza fursa za kiuchumi.

spot_img

Latest articles

Ofisi ya Msajili wa Hazina yatoa wito wa utawala bora kuimarisha uwekezaji wa umma

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH) imesisitiza kuwa mustakabali wa mafanikio...

TTB yamkaribisha bingwa wa Masumbwi duniani Terence kwa ziara ya utalii

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Ephraim Mafuru, amemkaribisha nchini...

DAWASA yasisitiza matumizi ya bidhaa za ndani kuimarisha huduma ya maji

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

DCEA yateketeza kilo 504.36 za Heroin Mtwara

Na Mwandishi Wetu, Mtwara MAMLAKa ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imeteketeza...

More like this

Ofisi ya Msajili wa Hazina yatoa wito wa utawala bora kuimarisha uwekezaji wa umma

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH) imesisitiza kuwa mustakabali wa mafanikio...

TTB yamkaribisha bingwa wa Masumbwi duniani Terence kwa ziara ya utalii

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Ephraim Mafuru, amemkaribisha nchini...

DAWASA yasisitiza matumizi ya bidhaa za ndani kuimarisha huduma ya maji

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...