Yanga yafuta taarifa ya ufafanuzi wa milioni 100, Chadema yawajia juu viongozi wa klabu

Na Mwandishi Wetu

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimewataka viongozi wa klabu ya  Yanga, kutathmini uhalali wao wa kuongoza klabu hiyo kwa kitendo cha kukichangia Chama Cha Mapinduzi (CCM)  sh 100 milioni.

Taarifa ya Chadema iliyotolewa leo tarehe 15 Agosti 2025, na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa  Chadema, Brenda Rupia.

Katika taarifa hiyo Rupia ameeleza kuwa kitendo cha Yanga kuichangia CCM ni dharau kwa wanachama na mashabiki wenye itikadi za vyama mbalimbali za siasa.

Rupia ameeleza kuwa taarifa ya yanga ya kudai kuwa mchango huo ulitoka kwa GSM haikuwa ya kweli kwa kuwa taarifa za awali zilidai kuwa GSM, amechangia sh.10 Bilioni, huku Yanga ikichangia sh.100 milioni.

Katika hatua nyingine Yanga imeondoa katika mitandao yake ya kijamii  taarifa ya ufafanuzi waliyoandika kwa Umma jana juu ya mchango huo, pamoja na kuwaomba radhi mashabiki waliyoitoa jana Agosti 14,2025.

spot_img

Latest articles

Ndejembi ataka Ewura kukagua maghala ya mafuta kuhakikisha hakuna mafuta yanayofichwa

📌Asema nchi ina usalama mkubwa wa mafuta hivyo wananchi waendelee kupata huduma muda wote 📌Timu...

Tanesco yagusa mioyo ya watoto wenye mahitaji maalum

📌Ni sehemu ya uwajibikaji wake kwa jamii 📌Yatoa misaada mbalimbali kwa vituo vitatu Dar...

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

More like this

Ndejembi ataka Ewura kukagua maghala ya mafuta kuhakikisha hakuna mafuta yanayofichwa

📌Asema nchi ina usalama mkubwa wa mafuta hivyo wananchi waendelee kupata huduma muda wote 📌Timu...

Tanesco yagusa mioyo ya watoto wenye mahitaji maalum

📌Ni sehemu ya uwajibikaji wake kwa jamii 📌Yatoa misaada mbalimbali kwa vituo vitatu Dar...

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...