Doyo wa NLD achukua fomu INEC ya kuwania Urais

Na Mwandishi Wetu

MGOMBEA Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha National League for Democracy (NLD), Doyo Hassan Doyo, leo ameambatana na mgombea mwenza wake, Chausiku Khatibu Mohamed, kufika katika ofisi za Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) kwa ajili ya kuchukua fomu za uteuzi.

Fomu hizo za kuomba kuteuliwa kuwania nafasi ya Rais na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia tiketi ya Chama cha NLD zilikabidhiwa rasmi na Jaji wa Mahakama ya Rufani, Jacobs Mwambegele.

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuchukua fomu, Doyo amesisitiza dhamira yake ya kupunguza matumizi makubwa ya serikali iwapo atapewa ridhaa ya kuiongoza nchi.

Ameeleza kuwa moja ya hatua atakazochukua ni kupunguza matumizi ya magari ya kifahari kwa viongozi wa umma, akisema.

“Nimekuja kuchukua fomu ya uteuzi kwa kutumia bajaji leo, kama ishara ya kuwaunga mkono vijana wanaoishi maisha ya kawaida na wanaojitahidi kujikwamua kupitia kazi zao za ujasiriamali. Wastani wa maisha yao unapaswa kueleweka na kuungwa mkono na kila mmoja wetu, kuna haja ya kupunguza matumizi serikani ili tuwaunge mkono vijana wengi zaidi.”

Kwa upande wake, Mgombea Mwenza wa Urais, Chausiku Khatibu Mohamed, amewashukuru wanachama wa NLD na Watanzania kwa ujumla kwa kuonesha imani, mshikamano na moyo wa kizalendo katika kipindi muhimu cha kuelekea Uchaguzi Mkuu.

“Tunaamini kuwa kwa pamoja tunaweza kuleta mabadiliko chanya kwa taifa letu, huku tukiweka msingi wa amani na mshikamano wa kweli. Amani ndiyo nguzo na tunu ya taifa letu. Chama cha NLD kimejipanga kufanya kampeni za kistaarabu, bila kudhalilisha wala kutweza utu wa mtu yeyote,” amesema.

spot_img

Latest articles

Ofisi ya Msajili wa Hazina yatoa wito wa utawala bora kuimarisha uwekezaji wa umma

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH) imesisitiza kuwa mustakabali wa mafanikio...

TTB yamkaribisha bingwa wa Masumbwi duniani Terence kwa ziara ya utalii

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Ephraim Mafuru, amemkaribisha nchini...

DAWASA yasisitiza matumizi ya bidhaa za ndani kuimarisha huduma ya maji

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

DCEA yateketeza kilo 504.36 za Heroin Mtwara

Na Mwandishi Wetu, Mtwara MAMLAKa ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imeteketeza...

More like this

Ofisi ya Msajili wa Hazina yatoa wito wa utawala bora kuimarisha uwekezaji wa umma

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH) imesisitiza kuwa mustakabali wa mafanikio...

TTB yamkaribisha bingwa wa Masumbwi duniani Terence kwa ziara ya utalii

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Ephraim Mafuru, amemkaribisha nchini...

DAWASA yasisitiza matumizi ya bidhaa za ndani kuimarisha huduma ya maji

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...