Januari Makamba hayumo, Nape apeta uteuzi CCM

Na Mwandishi wetu

Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Amos Makalla amejata majina ya wagombea sita wa  Jimbo Bumbuli mkoani Tanga  ambapo  aliyekuwa Mbunge wa Jimbo hilo kipindi kilichopita  Januari Makamba jina lake halijapita.

Makalla ametaja orodha ya majina ya wateule wa jimbo hilo watakaokwenda kupigiwa kura za maoni leo Julai 29,2025, jijini Dodoma, ambao ni Hidaya Kilima, Zahoro Rashid Hanuna, Eng. Ramadhan Singano, Rashid Salimu, Silas Joram na John Aloyce.

Kwa upande wake aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Mtama mkoani Lindi, Nape Nnauye atachuana na wagombea watatu ambao ni Jemedari Said, Jabiri Chilumba na Metta Nahonyo katika kulitetea Jimbo

Aidha aliyekuwa kada wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Ester Matiko, amepenya katika katika kinyang’anyiro cha kura za maoni, Jimbo la Tarime Mjini mkoani Mara akiwa miongoni mwa wagombea sita walioteuliwa.

spot_img

Latest articles

Tamasha la Singeli Agosti 2 wasanii kutoa burudani ya Kimataifa

Na Winfrida Mtoi Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Gerson Msigwa,...

Maandalizi ya Mkutano Mkuu Maalum UVCCM yamekamilika

Pichani ni Viongozi wa sekretarieti ya Umoja wa Vijana CCM wakikabidhi vifaa mbalimbali wezeshi...

INEC: Hakuna atakayeachwa nyuma kwenye Uchaguzi Mkuu 2025

Na Tatu Mohamed TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imesema imeweka mazingira wezeshi...

Serikali yawataka wakuu taasisi za umma kutengeneza mazingira rafiki ya kazi

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imewataka wakuu wa taasisi za umma kutengeneza mazingira rafiki ya...

More like this

Tamasha la Singeli Agosti 2 wasanii kutoa burudani ya Kimataifa

Na Winfrida Mtoi Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Gerson Msigwa,...

Maandalizi ya Mkutano Mkuu Maalum UVCCM yamekamilika

Pichani ni Viongozi wa sekretarieti ya Umoja wa Vijana CCM wakikabidhi vifaa mbalimbali wezeshi...

INEC: Hakuna atakayeachwa nyuma kwenye Uchaguzi Mkuu 2025

Na Tatu Mohamed TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imesema imeweka mazingira wezeshi...