Kenya yajiondoa  mashindano ya  CECAFA 

Na Mwandishi Wetu

Timu ya Taifa ya Kenya ‘Harambee Stars’ imejiondoa katika mashindano maalumu ya CECAFA  yaliyopangwa kuanza leo Julai 21,2025 jijini Arusha  kwa ajili  ya maandalizi ya   michuano ya Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ndani (CHAN- 2024).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Shirikisho la  Soka nchini Kenya (FKF), uamuzi huo umefanyika kutokana na  mapendekezo na ushauri wa benchi la ufundi la timu hiyo, likiongozwa na Kocha Mkuu Benni McCarthy, baada ya tathmini ya kina ya hali iliyopo kwa sasa, ikiwamo kutoridhishwa na mazingira.

Kenya ilikuwa icheze leo dhidi ya Uganda lakini baada ya kujitoa, itarejea nchini Kenya na kuendelea na maandalizi ya CHAN.

Mashindano hayo maalum yalikuwa yashirikishe  nchi nne za Tanzania, Uganda, Senegal na Kenya.

Michuano ya CHAN inatarajiwa kuanza  Agosti 2, 2025 ambapo Tanzania itafungua   dimba dhidi ya Burkina Faso kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam. 

spot_img

Latest articles

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

More like this

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...