Kenya yajiondoa  mashindano ya  CECAFA 

Na Mwandishi Wetu

Timu ya Taifa ya Kenya ‘Harambee Stars’ imejiondoa katika mashindano maalumu ya CECAFA  yaliyopangwa kuanza leo Julai 21,2025 jijini Arusha  kwa ajili  ya maandalizi ya   michuano ya Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ndani (CHAN- 2024).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Shirikisho la  Soka nchini Kenya (FKF), uamuzi huo umefanyika kutokana na  mapendekezo na ushauri wa benchi la ufundi la timu hiyo, likiongozwa na Kocha Mkuu Benni McCarthy, baada ya tathmini ya kina ya hali iliyopo kwa sasa, ikiwamo kutoridhishwa na mazingira.

Kenya ilikuwa icheze leo dhidi ya Uganda lakini baada ya kujitoa, itarejea nchini Kenya na kuendelea na maandalizi ya CHAN.

Mashindano hayo maalum yalikuwa yashirikishe  nchi nne za Tanzania, Uganda, Senegal na Kenya.

Michuano ya CHAN inatarajiwa kuanza  Agosti 2, 2025 ambapo Tanzania itafungua   dimba dhidi ya Burkina Faso kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam. 

spot_img

Latest articles

Rasmi Kocha Yanga afungashiwa virago usiku

Na Mwandishi Wetu Uongozi wa Klabu ya Yanga umevunja mkataba na Kocha Mkuu, Romain Folz. ...

Mwanamke ashikiliwa  Polisi kwa  kumuua mume wake na kumfukia ndani ya nyumba yao

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita linamshikilia mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina...

Padre aliyepotea apatikana akiwa hai

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi mkoani Ruvuma limefanikiwa kumpata Padre Camillus Nikata wa Jimbo...

More like this

Rasmi Kocha Yanga afungashiwa virago usiku

Na Mwandishi Wetu Uongozi wa Klabu ya Yanga umevunja mkataba na Kocha Mkuu, Romain Folz. ...

Mwanamke ashikiliwa  Polisi kwa  kumuua mume wake na kumfukia ndani ya nyumba yao

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita linamshikilia mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina...