Gwajima: Sitanyamaza watu wakiendelea kutekwa, tuwape Chadema ‘Reform’ ili Taifa lisonge mbele

Na Mwandishi Wetu

MBUNGE wa Kawe anayemaliza muda wake na Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima, amesema hawezi kukaa kimya endapo vitendo vya utekaji vitaendelea nchini, huku akisisitiza kuwa bado ni mwanachama thabiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Akizungumza na waandishi wa habari leo Julai 16, 2025, Askofu Gwajima amesema licha ya baadhi ya watu kumtuhumu kwamba ana nia ya kuhamia vyama vya upinzani, yeye bado yupo CCM kwa dhati na hatarajii kutoka, bali atasimama ndani ya chama hicho kutetea ukweli.

“Siwezi kuacha kuzungumza kama watu wataendelea kutekwa. Nipo CCM na nitaendelea kuwepo. Hakuna kutoka wala kugombana, tutabanana humu humu na tutaendelea kushauriana,” amesema Askofu Gwajima.

Hata hivyo, Askofu Gwajima amesisitiza kuwa hajawahi kusema kama CCM ndiyo inateka watu, lakini kama chama kilicho madarakani, kina wajibu wa kuhakikisha haki, amani na maridhiano vinapatikana nchini.

Akizungumzia msimamo wa Chadema kuhusu kutoshiriki Uchaguzi Mkuu bila kufanyika kwa mabadiliko ya mfumo wa uchaguzi (reforms), Askofu Gwajima amesema ni busara kwa CCM kama chama tawala kuhakikisha maridhiano yanapatikana ili Taifa lisigawanyike.

“Tunaweza kushinda uchaguzi bila Chadema, lakini je, tutawezaje kuitawala nchi iliyogawanyika kwa misingi ya uchaguzi usioaminika? Ni bora tukakubaliana kwenye baadhi ya reforms, tukaingia wote, kisha tuwashinde kwenye uwanja wa haki,” amesema.

Askofu Gwajima amesema si busara kuendekeza ushindi wa kisiasa kwa gharama ya mshikamano wa kitaifa, na kuhimiza CCM kutanguliza maslahi ya Taifa kabla ya maslahi ya kisiasa.

“Tuwe na nchi iliyoungana baada ya uchaguzi. Hapo ndipo Rais anaweza kuongoza kwa amani na kuleta maendeleo. Nchi huja kwanza, vyama vinakuja baadaye,” ameongeza.

Ameishauri CCM na Serikali kutafuta njia ya busara ya kuafikiana na Chadema kuhusu madai ya reform, kwa lengo la kupata ushindani wa haki na taifa lenye mshikamano baada ya uchaguzi.

spot_img

Latest articles

Dk. Mwigulu: Tutamuenzi kwa vitendo marehemu Jenista

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itayaendeleza mambo yote mema yaliyofanywa na...

Balozi Bandora kuzikwa kesho makaburi ya Kinondoni

Mwanadiplomasia nguli wa Tanzania, aliyewahi  kuwa Balozi wa Tanzania nchini Nigeria na Mratibu Mkazi...

Serikali yajipanga kuimarisha utumishi wa umma, kuendeleza mageuzi ya kidigitali

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa...

Bokya amtahadharisha mapema Tyson wa Bongo

Na Winfrida Mtoi Bondia Ismail Khalid maarufu Boyka ametamba kutoa kipigo kikali kwa mpinza wake...

More like this

Dk. Mwigulu: Tutamuenzi kwa vitendo marehemu Jenista

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itayaendeleza mambo yote mema yaliyofanywa na...

Balozi Bandora kuzikwa kesho makaburi ya Kinondoni

Mwanadiplomasia nguli wa Tanzania, aliyewahi  kuwa Balozi wa Tanzania nchini Nigeria na Mratibu Mkazi...

Serikali yajipanga kuimarisha utumishi wa umma, kuendeleza mageuzi ya kidigitali

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa...