Warning: Array to string conversion in /home/themedia/domains/themediabrains.com/public_html/wp-includes/shortcodes.php on line 434
Array

Bashe: Hakuna vanila inayouzwa milioni 1 kwa kilo

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe ametoa rai kwa wananchi kuwa na utaratibu wa kufuatilia bei ya mazao katika mitandao mbalimbali ya kimataifa ili kuepuka uzushi unaoweza kujitokeza kwenye baadhi ya bei za mazao.

Waziri Kilimo, Hussein Bashe.

Hayo ameyasema September 3, 2023 jijini Dar es Salaam wakati wa mkutano wa wahariri ulioandaliwa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Zuhura Yunus Ikulu wenye lengo la kujadili kuhusu mkutano mkubwa wa mifumo ya chakula Afrika AGRF unaotarajiwa kufanyika Septemba 5 hadi 8, mwaka huu kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC).

Amesema Watanzania wengi walikuwa wakiaminishwa kuhusu kilimo cha vanila kwamba kilo moja inaweza kuuzwa kwa Sh million 1 hadi 1.5 jambo ambalo siyo kweli.

“Watanzania wanapaswa kupuuza taarifa hizo ambazo zimekuwa zikitangazwa katika mitandao mbalimbali siyo kweli hiyo bei haipo hata kama ni kweli nchi ilikuwa na uhitaji wa zao hilo,” amesema Bashe.

Ameongeza kuwa Serikali hivi karibuni itatoa muongozo kuhusu zao hilo ambalo kwasasa linalimwa katika mikoa mbalimbali ikiwa ikiwamo Kagera na Kilimanjaro.

Amesema ni kweli Tanzania ilikuwa na uhitaji wa zao hilo na kwamba hiyo ni kutokana na nchi ambazo zinaongoza kwa kulima zao hilo kukumbwa na majanga mbalimbali.

“Ni kweli tulikuwa na uhitaji wa zao hilo kutokana na nchi kama Madagascar ambao ndiyo wakulima wakuu wa zao hilo ilikumbwa na kimbunga lakini siyo chanzo cha kufikia bei ya Sh milioni moja kwa kilo huo ni udanganyifu, Watanzania waupuuze wasubiri Serikali itatoa muongozo kuhusu zao hilo,” amesema. 

spot_img

Latest articles

Fountain Gate yatoa kocha bora

Na Mwandishi Wetu Kocha wa timu ya Fountain Gate,  Mohamed Laizer amechaguliwa kuwa kocha bora...

Nyota JKT Queens aipigia hesabu Asec Mimosa

Na Winfrida Mtoi Mshambuliaji wa JKT Queens FC, Jamila Rajabu, amesema  amejipanga  kutengeneza  nafasi na...

Zungu achaguliwa kuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Na Mwandishi Wetu MBUNGE mteule wa Jimbo la Ilala Mussa Azzan Zungu ameibuka mshindi...

Heche viongozi wengine Chadema waachiwa na Polisi kwa dhamana

Na Mwandishi Wetu Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), John Heche na...

More like this

Fountain Gate yatoa kocha bora

Na Mwandishi Wetu Kocha wa timu ya Fountain Gate,  Mohamed Laizer amechaguliwa kuwa kocha bora...

Nyota JKT Queens aipigia hesabu Asec Mimosa

Na Winfrida Mtoi Mshambuliaji wa JKT Queens FC, Jamila Rajabu, amesema  amejipanga  kutengeneza  nafasi na...

Zungu achaguliwa kuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Na Mwandishi Wetu MBUNGE mteule wa Jimbo la Ilala Mussa Azzan Zungu ameibuka mshindi...