Rais Samia azindua kiwanda cha kutengeneza mabomba ya maji na uchakataji Pamba

Mwandishi Wetu

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, leo Juni 16, 2025, amezindua kiwanda cha kutengeneza mabomba ya maji na uchakataji wa pamba cha MOLI Oil Mills Co. Ltd kilichopo Bariadi, Mkoa wa Simiyu.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, amesema hatua hiyo itasaidia kuongeza ajira lakini pia pamba inayozalishwa ndani ya nchi kutumika hapa nchini kuzalisha bidhaa nyingine badala ya kuisafirisha nje ya nchi kama ambavyo inavyofanyika sasa.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan akimsikiliza Mkurugenzi wa Kiwanda cha MOLI Oil Mills Co. Ltd, Milembe Gugu Silanga kuhusu utengenezaji wa mabomba ya maji na uchakataji wa pamba kabla ya ufunguzi wa kiwanda hicho Bariadi mkoani Simiyu leo Juni 16 Juni, 2025.

“Tunajua kwamba Simiyu zao kubwa la kiuchumi ni pamba ukiacha mengine na nimshukuru mwekezaji hapa wa ndani amewaza kuongeza thamani angalau kwa hatua ya kwanza, lakini hatua ya pili sasa tutanunua kwake kuweka kwenye kiwanda ambacho tayari tumeanza kukijenga cha kutengeneza nyuzi za pamba.

“ Tunataka kusitisha kupeleka pamba yetu kama ilivyo kwenye marobota kwa wenzetu wakatengeneze nguo na watu wao wapate kazi, tunataka pamba yetu tuitengeneze hapa hapa ili watu wetu wa Simiyu waweze kupata ajira ndani ya mkoa huu,” amesema Rais Samia.


spot_img

Latest articles

Rais Samia: MEATU mtaendelea kupata miradi mikubwa ya maendeleo ikiwemo Nishati

📌Asema baada ya Vijiji vyote Meatu kupata umeme kasi inaelekea vitongojini 📌 Ataka umeme utumike...

GFA yaweka rekodi uundaji magari nchini, yakamilisha gari ya 4000

Na Mwandishi Wetu Kiwanda cha kwanza kutengeneza na kuunganisha magari Tanzania cha GF Vehicles Assemblers...

Mwanafunzi wa chuo ashikiliwa Polisi kwa kumuua mwenzake  wakiwa ‘Club’ wamelewa

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha...

Mwanamke ajiua kwa sumu  kisa mapenzi

Na Mwandishi Wetu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Kamishna Msaidizi Richard Abwao,  amesema mwanamke mmoja...

More like this

Rais Samia: MEATU mtaendelea kupata miradi mikubwa ya maendeleo ikiwemo Nishati

📌Asema baada ya Vijiji vyote Meatu kupata umeme kasi inaelekea vitongojini 📌 Ataka umeme utumike...

GFA yaweka rekodi uundaji magari nchini, yakamilisha gari ya 4000

Na Mwandishi Wetu Kiwanda cha kwanza kutengeneza na kuunganisha magari Tanzania cha GF Vehicles Assemblers...

Mwanafunzi wa chuo ashikiliwa Polisi kwa kumuua mwenzake  wakiwa ‘Club’ wamelewa

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha...