Ndege ya Air India yaanguka, ikiwa na abiria  242

Na Mwandishi Wetu

Ndege ya abiria ya Shirika la Ndege la  India ‘Air India’  iliyokuwa inatokea nchini India kwenda London nchini Uingereza imeanguka na kuwaka moto leo Juni 12, 2025 katika eneo la Ahmedabad India muda mfupi baada ya kupaa ikiwa na watu 242.

Kwa mujibu wa taarifa za mamlaka nchini India zimesema ndege hiyo ilikuwa imebeba  abiria 169 ni raia wa India,  raia wa  53 Uingereza, Wareno saba na raia wa Canada mmoja, huku wafanyakazi wa ndege hiyo  ni 12.

Waziri Mkuu wa India Narendra Modi  kupitia mtandao wake wa kijamii wa X, amesema ameshtushwa sana na ajali hiyo ya ndege.

“Ajali ya Ahmedabad imetushtua na kutuhuzunisha. Haielezeki jinsi inavyovunja moyo, amesema Modi katika ujumbe huo alioandika.

Mtandao wa kufuatilia safari za ndege wa Flightradar24 umesema ndege hiyo ilikuwa aina ya Boeing 787-8 Dreamliner, mojawapo ya ndege za kisasa zaidi zinazotumika.

spot_img

Latest articles

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

Serikali: Tuchukue hatua kuepuka madhara ya usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa (UVIDA)

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia kwa Mkurugenzi msaidizi, Kitengo cha Afya Moja, Ofisi ya...

Serikali yawaita wadau kujitokeza kusapoti ushiriki wa wanawake michezoni

Na Winfrida Mtoi Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma 'MwanaFA' amewaomba...

More like this

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

Serikali: Tuchukue hatua kuepuka madhara ya usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa (UVIDA)

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia kwa Mkurugenzi msaidizi, Kitengo cha Afya Moja, Ofisi ya...