Raia wa Nchi 72 kuingia Tanzania bila Viza

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

SERIKALI imeingia makubaliano na nchi mbalimbali ili kurahisisha utaratibu wa viza ambapo raia wa nchi 71 hawahitaji viza wanapoingia nchini.

Kwa sasa watalii kutoka mataifa mengi zaidi duniani wanaruhusiwa kupata visa wanapowasili (visa on arrival) kwenye viwanja vya ndege vya kimataifa kama Julius Nyerere (Dar es Salaam), Kilimanjaro na Zanzibar.

Haya yamebainishwa na Naibu Waziri wa Maliasili na Ualii, Dunstan Kitandula(Mb) alipokuwa akijibu swali la Dkt. Pius Stephen Chaya aliyetaka kujua ni jitihada gani zimefanyika kurahisisha upatikanaji wa VISA kwa Watalii wenye uraia tofauti wanaokuja nchini kwa mwitikio wa Tanzania the Royal Tour.

Aidha Kitandula aliongeza kuwa Serikali imeendelea kuboresha utaratibu wa utoaji wa viza nchini ili kuendana na mabadiliko ya teknolojia duniani.

Mathalan, Serikali kupitia Idara ya Uhamiaji imeanzisha mfumo wa maombi ya viza kwa njia ya mtandao (e-Visa) unaowawezesha watalii kuomba viza popote walipo duniani bila kulazimika kufika ubalozini.

“Halikadhalika, Serikali imeboresha Kanuni za Uhamiaji za mwaka 2023 (GN 428) ambapo kwa sasa watalii wanaotumia Visitors Pass wanaruhusiwa kutembelea Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki na kurejea Tanzania bila hitaji la kuomba upya pasi ya kuingia nchini,” alisema Kitandula.

Suala la visa lina uhusiano wa moja kwa moja na sekta ya utalii, Wizara ya Maliasili na Utalii imeimarisha ushirikiano na Wizara ya Mambo ya Ndani, hususan Idara ya Uhamiaji, katika nyanja mbalimbali ikiwemo ukusanyaji wa takwimu za watalii na kuwa na mikakati ya pamoja ya kuvutia watalii na fursa za uwekezaji.

Hivi karibuni, Wizara kupitia Chuo cha Taifa cha Utalii imetoa mafunzo ya Huduma kwa Wateja na Ukarimu kwa Maafisa wa Jeshi la Uhamiaji ili kuboresha huduma zinazotolewa kwa wageni wanaoingia nchini, ikiwemo watalii.

spot_img

Latest articles

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...

Tanesco yazindua ndege nyuki (Drones) kuboresha miundombinu ya umeme nchini

📌Ni sehemu ya utekelezaji wa mikakati yake kuimarisha huduma kwa wateja kwa kutumia njia...

More like this

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...