Warning: Array to string conversion in /home/themedia/domains/themediabrains.com/public_html/wp-includes/shortcodes.php on line 434
Array

Huu ndiyo mwelekeo mpya wa Tanesco

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Waziri wa Nishati, January Makamba, amesema mabadiliko yanayofanywa katika Shirika la Umeme Nchini (Tanesco) yameleta mafanikio makubwa kuwahi kutokea tangu kuanzishwa kwake.

Kwa mwaka 2021/22 shirika hilo limerekodi mapato ya Sh trilioni 2.3, faida ya Sh bilioni 109.4 huku thamani ya mali ikifikia Sh trilioni 19.

Akizungumza Julai 31,2023 wakati wa uzinduzi wa taarifa ya mwaka 2021/22 na mpango mkakati wa miaka 10 ijayo, amesema dhamana ya shirika hilo kwa maendeleo ya nchi ni kubwa hivyo lazima lifanye mambo makubwa.

“Shilingi bilioni 109 ni faida ya kihistoria, tumepata mafanikio lakini safari bado ni ndefu sana, lakini dalili ni nzuri.

“Tunaomba subira, mtupe muda kwa sababu mabadiliko yanachukua muda mrefu…mabadiliko yanayofanyika Tanesco yanaweza yasieleweke mwanzoni, itabidi tuzoee namna ambavyo mambo yanafanyika,” amesema Makamba.

Hata hivyo amesema faida iliyopatikana haitoshelezi hivyo bado wataendelea kutegemea mtaji wa Serikali na sekta binafsi katika uwekezaji wa umeme.

Naye Msajili wa Hazina, Nehemia Mchechu, amesema kutokana na mabadiliko iliyoyafanya Tanesco kuanzia Septemba mwaka huu itarudishiwa mamlaka yake ya kuweza kuajiri na kushughulikia masuala ya masilahi.

Hata hivyo ametahadharisha uhuru huo uwe wa uwazi na uwajibikaji kwa kuzingatia vigezo walivyokubaliana.

“Mabadiliko ya utendaji katika taasisi zetu ni jambo lisiloepukika, tusipofanya marekebisho kila siku tutakuwa watu wa kunyosheana vidole na lazima tubadilike katika hilo.

“Kila taasisi lazina wajitahidi kuwa wazi, kuwasilisha ripoti za mwaka na kuwa na mikakati na kuiwasilisha,” amesema Mchechu.

Mwanzilishi na Mkurugenzi Mtendaji wa Lindam Group, Zuhura Muro, ameshauri Tanesco iendelee kuhakikisha nishati inapatikana kwa gharama nafuu na kuwafikia wananchi wengi hasa wanawake ili waweze kuzalisha na kuchangia pato la taifa zaidi.

Mkurugenzi wa Tanesco, Maharage Chande, amesema kutokana na mikakati waliyonayo wanaamini kufikia mwaka 2026/27 matatizo mengi yatakuwa yamekwisha.

spot_img

Latest articles

Kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani: TRA Yakabidhi Vifaa Tiba Vyenye Thamani ya Milioni 40

Na Tatu Mohamed KUELEKEA maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yanayoadhimishwa kila mwaka Machi 8,...

UWT Makangarawe watoa msaada kwa watoto wenye mahitaji maalum kuelekea Siku ya Wanawake Duniani

Na Tatu Mohamed KATIKA kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, Umoja wa Wanawake...

‘Makomandoo’ wazitia hasara Simba na Yanga

Na Mwandishi Wetu KLABU za Simba na Yanga zimetozwa faini ta sh.5,000,000 kila moja kwa...

Mwamuzi aliyekataa bao la Simba Zanzibar afungiwa

Na Mwandishi Wetu MWAMUZI Kassim Mpanga Mpanga wa Dar es Salaam, amefungiwa miezi sita  kosa...

More like this

Kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani: TRA Yakabidhi Vifaa Tiba Vyenye Thamani ya Milioni 40

Na Tatu Mohamed KUELEKEA maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yanayoadhimishwa kila mwaka Machi 8,...

UWT Makangarawe watoa msaada kwa watoto wenye mahitaji maalum kuelekea Siku ya Wanawake Duniani

Na Tatu Mohamed KATIKA kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, Umoja wa Wanawake...

‘Makomandoo’ wazitia hasara Simba na Yanga

Na Mwandishi Wetu KLABU za Simba na Yanga zimetozwa faini ta sh.5,000,000 kila moja kwa...