Msajili hazina aongoza mazungumzo ya uwekezaji na kampuni ya Uswisi

Na Mwandishi Wetu, Abidjan

MSAJILI wa Hazina, Nehemiah Mchechu, Mei 14, 2025, ameongoza mazungumzo ya kitaalamu kati ya Serikali ya Tanzania na Soren Toft, Afisa Mtendaji Mkuu wa Mediterranean Shipping Company (MSC), kuhusu uwekezaji wa kimkakati katika Bandari ya Dar es Salaam na Mangapwani–Zanzibar.

Mazungumzo hayo na kampuni ambayo makao yake makuu yapo Geneva, Uswisi, yamefanyika jijini Abidjan, Côte d’Ivoire pembezoni mwa Jukwaa la Maafisa Watendaji Wakuu Afrika, yakilenga fursa za kuboresha huduma na miundombinu ya bandari hizo mbili muhimu kwa uchumi wa taifa na ukanda wa Afrika Mashariki.

Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), kupitia kwa Mkurugenzi wa Fedha na Utawala, Pascal Maganga, kimeihakikishia MSC kuwa kipo tayari kushirikiana kikamilifu kwa kuhakikisha mazingira rafiki ya uwekezaji ili uwekezaji huo ufanyike kwa mafanikio makubwa.

Kwa upande wake, Toft ameonyesha dhamira ya dhati ya MSC kushirikiana na Tanzania katika kuimarisha miundombinu ya bandari, akisisitiza umuhimu wa Bandari ya Dar es Salaam na Mangapwani kama lango kuu la biashara kwa ukanda wa Afrika Mashariki.

Tanzania inaendelea kujidhihirisha kama kitovu cha uwekezaji barani Afrika, kwa kushirikiana na wadau wakubwa wa kimataifa katika kuendeleza miradi ya kimkakati itakayochochea uchumi wa nchi na ajira kwa wananchi.

spot_img

Latest articles

Ndumbaro: Sheria 300 Zimetafsiriwa kwa Kiswahili Ili Kuimarisha Uelewa kwa Wananchi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Katiba na Sheria, Dkt. Damas Ndumbaro, amesema kuwa hadi...

Jessica: CCM inajali uongozi wa vijana

Na Mwandishi Wetu KATIBU wa Idara ya Uhamasishaji na Chipukizi UVCCM TAIFA, Jessica Mshama...

Waziri Aweso: Tuna uhakika wa maji ya kutosha Dar na Pwani

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso amewatoa hofu wakazi wa mikoa ya...

PURA yajivunia mafanikio katika Ajenda ya Nishati Safi na ushiriki wa Watanzania Sekta ya Mafuta na Gesi

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Kudhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) imesema inajivunia...

More like this

Ndumbaro: Sheria 300 Zimetafsiriwa kwa Kiswahili Ili Kuimarisha Uelewa kwa Wananchi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Katiba na Sheria, Dkt. Damas Ndumbaro, amesema kuwa hadi...

Jessica: CCM inajali uongozi wa vijana

Na Mwandishi Wetu KATIBU wa Idara ya Uhamasishaji na Chipukizi UVCCM TAIFA, Jessica Mshama...

Waziri Aweso: Tuna uhakika wa maji ya kutosha Dar na Pwani

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso amewatoa hofu wakazi wa mikoa ya...