TFF kuja mshirika wa kubashiri mechi zake

Na Mwandishi Wetu

Shirikisho wa Soka Tanzania(TFF),limesema kuanzia msimu ujao wa 2025/2026 litakuwa na mshirika wa michezo ya kubashiri(kubeti) katika mashindano yake yote.

Kwa mujibu wa taarifa ya TFF  waliyotoa leo, Mei 12, 2025 mshirika huyo atashikilia haki hizo kwa kipindi chote cha makubaliano, hivyo yeyote mwenye nia au kuhitaji ‘Odds’ kwa ajili ya mechi ambazo zitakuwa chini ya TFF atalazimika kuwasiliana na mshirika huyo.

“Makubaliano yetu na mshirika huyo yatakuwa ni kwa ajili ya odds tu na si ushirika mwingine na kampuni za michezo ya kubashiri(betting companies) kama udhamini(sponsorship) au ushirikiano,” imesema taarifa hiyo kwa umma.

Taarifa hiyo imesema kuwa utaratibu huo ndio unaotumika katika ligi mbalimbali barani Ulaya, ikieleza kuwa itazinufaisha kimapato klabu mechi zao zitakuwa zimeingia kwenye odds.

“Licha ya malipo yatakayokuwa yanatokana na odds, bado klabu zitaendelea kudhaminiwa na kampuni hizo michezo ya kubashiri, kwani utaratibu huu hauathiri makubaliano ya udhamini kati ya pande hizo.

“Utaratibu wa kumpata mshirika huyo utafanyika kwa njia ya mnada utakaotangazwa  wakati wa utakapowadia,” imesema.

spot_img

Latest articles

Kamati ya kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini yaipongeza Tanesco utekelezaji wa Mradi wa Umeme Jua Kishapu

📌 Watembelea mradi kuona ufanisi wake 📌 Shilingi bilioni 118 zatumika kutekeleza mradi 📌 Watoa rai...

Kamati ya kudumu ya Binge Nishati na Madini yaridhishwa na maendeleo ya Kiwanda cha nguzo za zege

📌Ni mradi wa kihistoria kutekelezwa chini ya Serikali ya awamu ya Sita 📌 Yaipongeza...

Waziri Ulega, RC Chalamila pekueni mafaili wizarani

KWA nyakati tofauti viongozi wawili wamezungumzia jiji la Dar es Salaam kuhusu msongamano wa...

Rais Samia amuasili mtoto mchanga aliyetelekezwa Nzega

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ,Samia Suluhu Hassan, amemuasili mtoto...

More like this

Kamati ya kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini yaipongeza Tanesco utekelezaji wa Mradi wa Umeme Jua Kishapu

📌 Watembelea mradi kuona ufanisi wake 📌 Shilingi bilioni 118 zatumika kutekeleza mradi 📌 Watoa rai...

Kamati ya kudumu ya Binge Nishati na Madini yaridhishwa na maendeleo ya Kiwanda cha nguzo za zege

📌Ni mradi wa kihistoria kutekelezwa chini ya Serikali ya awamu ya Sita 📌 Yaipongeza...

Waziri Ulega, RC Chalamila pekueni mafaili wizarani

KWA nyakati tofauti viongozi wawili wamezungumzia jiji la Dar es Salaam kuhusu msongamano wa...