TFF kuja mshirika wa kubashiri mechi zake

Na Mwandishi Wetu

Shirikisho wa Soka Tanzania(TFF),limesema kuanzia msimu ujao wa 2025/2026 litakuwa na mshirika wa michezo ya kubashiri(kubeti) katika mashindano yake yote.

Kwa mujibu wa taarifa ya TFF  waliyotoa leo, Mei 12, 2025 mshirika huyo atashikilia haki hizo kwa kipindi chote cha makubaliano, hivyo yeyote mwenye nia au kuhitaji ‘Odds’ kwa ajili ya mechi ambazo zitakuwa chini ya TFF atalazimika kuwasiliana na mshirika huyo.

“Makubaliano yetu na mshirika huyo yatakuwa ni kwa ajili ya odds tu na si ushirika mwingine na kampuni za michezo ya kubashiri(betting companies) kama udhamini(sponsorship) au ushirikiano,” imesema taarifa hiyo kwa umma.

Taarifa hiyo imesema kuwa utaratibu huo ndio unaotumika katika ligi mbalimbali barani Ulaya, ikieleza kuwa itazinufaisha kimapato klabu mechi zao zitakuwa zimeingia kwenye odds.

“Licha ya malipo yatakayokuwa yanatokana na odds, bado klabu zitaendelea kudhaminiwa na kampuni hizo michezo ya kubashiri, kwani utaratibu huu hauathiri makubaliano ya udhamini kati ya pande hizo.

“Utaratibu wa kumpata mshirika huyo utafanyika kwa njia ya mnada utakaotangazwa  wakati wa utakapowadia,” imesema.

spot_img

Latest articles

Neema Mchau ajitosa kugombea Udiwani Viti Maalum Ilala

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Jukwaa la Wanawake Kata ya Gongolamboto Neema Mchau amechukua fomu...

Amanzi na Babu Tale uso kwa uso Jimboni

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Katibu wa Umoja wa Vijana wa CCM Tawi la Chuo...

VETA Pwani yabuni Mita ya Maji ya Kisasa, kutatua migogoro kwa wapangaji

Na Tatu Mohamed KATIKA hatua ya kuleta mageuzi katika usimamizi wa matumizi ya maji...

Ofisi ya Msajili Hazina yazitaka taasisi za umma kutumia maonesho ya Sabasaba kutangaza huduma

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili Hazina yazitaka taasisi za umma kutumia maonesho ...

More like this

Neema Mchau ajitosa kugombea Udiwani Viti Maalum Ilala

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Jukwaa la Wanawake Kata ya Gongolamboto Neema Mchau amechukua fomu...

Amanzi na Babu Tale uso kwa uso Jimboni

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Katibu wa Umoja wa Vijana wa CCM Tawi la Chuo...

VETA Pwani yabuni Mita ya Maji ya Kisasa, kutatua migogoro kwa wapangaji

Na Tatu Mohamed KATIKA hatua ya kuleta mageuzi katika usimamizi wa matumizi ya maji...