Simba azidi kumkimbiza Yanga,  bado pointi 4

Na Mwandishi Wetu

Simba imeibuka na ushindi wa mabao 5-1 dhidi ya Pamba Jiji katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa leo Mei 8,2025 kwenye Uwanja wa KMC Complex, jijini Dar es Salaam.

Katika mchezo huo mabao ya Simba yamefungwa na Jean Ahoua alifunga matatu ‘Hat trick’ na Lionel Ateba aliyefunga mawili, huku bao la Pamba likifungwa na Mathew Momanyi.

Ushindi huo unaifanya Simba kupunguza ‘gap’ la pointi ambapo imebakisha alama nne kuifikia Yanga iliyopo kileleni na pointi 70.

Simba imefikisha pointi 66 ikiwa imecheza michezo 25, wakati Yanga imecheza mechi 26.

Kwa upande wa Pamba hali inazidi kuwa ngumu kwao, kwani ipo katika hatari ya kushuka daraja ambapo inashika nafasi ya 13 katika msimamo na pointi 27, imecheza michezo 27.
 

spot_img

Latest articles

Neema Mchau ajitosa kugombea Udiwani Viti Maalum Ilala

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Jukwaa la Wanawake Kata ya Gongolamboto Neema Mchau amechukua fomu...

Amanzi na Babu Tale uso kwa uso Jimboni

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Katibu wa Umoja wa Vijana wa CCM Tawi la Chuo...

VETA Pwani yabuni Mita ya Maji ya Kisasa, kutatua migogoro kwa wapangaji

Na Tatu Mohamed KATIKA hatua ya kuleta mageuzi katika usimamizi wa matumizi ya maji...

Ofisi ya Msajili Hazina yazitaka taasisi za umma kutumia maonesho ya Sabasaba kutangaza huduma

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili Hazina yazitaka taasisi za umma kutumia maonesho ...

More like this

Neema Mchau ajitosa kugombea Udiwani Viti Maalum Ilala

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Jukwaa la Wanawake Kata ya Gongolamboto Neema Mchau amechukua fomu...

Amanzi na Babu Tale uso kwa uso Jimboni

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Katibu wa Umoja wa Vijana wa CCM Tawi la Chuo...

VETA Pwani yabuni Mita ya Maji ya Kisasa, kutatua migogoro kwa wapangaji

Na Tatu Mohamed KATIKA hatua ya kuleta mageuzi katika usimamizi wa matumizi ya maji...