Simba azidi kumkimbiza Yanga,  bado pointi 4

Na Mwandishi Wetu

Simba imeibuka na ushindi wa mabao 5-1 dhidi ya Pamba Jiji katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa leo Mei 8,2025 kwenye Uwanja wa KMC Complex, jijini Dar es Salaam.

Katika mchezo huo mabao ya Simba yamefungwa na Jean Ahoua alifunga matatu ‘Hat trick’ na Lionel Ateba aliyefunga mawili, huku bao la Pamba likifungwa na Mathew Momanyi.

Ushindi huo unaifanya Simba kupunguza ‘gap’ la pointi ambapo imebakisha alama nne kuifikia Yanga iliyopo kileleni na pointi 70.

Simba imefikisha pointi 66 ikiwa imecheza michezo 25, wakati Yanga imecheza mechi 26.

Kwa upande wa Pamba hali inazidi kuwa ngumu kwao, kwani ipo katika hatari ya kushuka daraja ambapo inashika nafasi ya 13 katika msimamo na pointi 27, imecheza michezo 27.
 

spot_img

Latest articles

Kamati ya kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini yaipongeza Tanesco utekelezaji wa Mradi wa Umeme Jua Kishapu

📌 Watembelea mradi kuona ufanisi wake 📌 Shilingi bilioni 118 zatumika kutekeleza mradi 📌 Watoa rai...

Kamati ya kudumu ya Binge Nishati na Madini yaridhishwa na maendeleo ya Kiwanda cha nguzo za zege

📌Ni mradi wa kihistoria kutekelezwa chini ya Serikali ya awamu ya Sita 📌 Yaipongeza...

Waziri Ulega, RC Chalamila pekueni mafaili wizarani

KWA nyakati tofauti viongozi wawili wamezungumzia jiji la Dar es Salaam kuhusu msongamano wa...

Rais Samia amuasili mtoto mchanga aliyetelekezwa Nzega

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ,Samia Suluhu Hassan, amemuasili mtoto...

More like this

Kamati ya kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini yaipongeza Tanesco utekelezaji wa Mradi wa Umeme Jua Kishapu

📌 Watembelea mradi kuona ufanisi wake 📌 Shilingi bilioni 118 zatumika kutekeleza mradi 📌 Watoa rai...

Kamati ya kudumu ya Binge Nishati na Madini yaridhishwa na maendeleo ya Kiwanda cha nguzo za zege

📌Ni mradi wa kihistoria kutekelezwa chini ya Serikali ya awamu ya Sita 📌 Yaipongeza...

Waziri Ulega, RC Chalamila pekueni mafaili wizarani

KWA nyakati tofauti viongozi wawili wamezungumzia jiji la Dar es Salaam kuhusu msongamano wa...